KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, February 12, 2010

Clinton afanyiwa upasuaji wa moyo




Bill Clinton alilazwa hospitalini baada ya kulalamika kwamba ana maumivu ya kifua. Madaktari wanasema amewekewa mipira miwili katika mishipa yake ya moyo ambayo ilikuwa imeanza kuziba ili kuifungua.
Inaarifiwa kuwa rais huyo wa zamani wa Marekani yuko katika hali nzuri. Mke wake, Hillary ambaye ni waziri wa mambo ya nje wa Marekani amesafiri kwenda New York ili kuwa naye.

Bwana Clinton, aliwahi kufanyiwa upasuaji wa mishipa inayopeleka damu moyoni mwaka 2004.

Kwa miaka ya hivi majuzi, aliandamana na kumuunga mkono mkewe Hillary katika kampeni yake ya urais na tangu kutokea kwa tetemeko la ardhi nchini Haiti, Clinton amekuwa akihudumu kama mjumbe maalum wa umoja wa mataifa wa taifa hilo.

No comments:

Post a Comment