KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Tuesday, December 8, 2009

Shambulio la bomu laua 118 Baghdad


Shambulio la bomu laua 118 Baghdad

Taarifa kutoka Iraq, zinaeleza kuwa watu zaidi ya 118 wameuawa katika mashambulio ya mabomu mjini Baghdad.
Inaarifiwa kuwa mabomu hayo yalikuwa yametegwa ndani ya magari yaliyokuwa yameegeshwa maeneo tofauti.

Mabomu hayo manne yalilipuka kwa wakati mmoja, la kwanza likilipuka karibu na kituo cha polisi eneo la Doura lenye waisilamu wengi wa Sunni.

Wenye kufanya mashambulizi hayo wanasemekana walilenga hasa ofisi za serikali au vyuo vikuu.

Wizara ya mambo ya ndani ni miongoni mwa majengo yaliyoshambuliwa. Hakuna aliyekiri kutega mabomu hayo.

No comments:

Post a Comment