KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Wednesday, November 25, 2009

Gaddafi 'kusuluhisha' mzozo wa Misri-Algeria


Gaddafi 'kusuluhisha' mzozo wa Misri-Algeria

Kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi amekubali kuwa mpatanishi katika mzozo kati ya Algeria na Misri,shirika la habari la serikali limesema.
Shirika la habari la Libya lijulikanalo kama Jana limeripoti kuwa Jumuiya ya Waarabu imemuomba Gaddafi kupatanisha mataifa hayo mawili.

Kila upande umeshtumu mashabiki wengine kwa kufanya ghasia baada ya mechi muhimu ya kuania kufuzu kwa fainali za kombe la dunia wiki iliyopita,ambapo Algeria ilishinda.

Wakati huo huo,takriban wasomi 150 wa Misri na Algeria wametoa wito wa kukomeshwa kwa mzozo huo.

No comments:

Post a Comment