KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Thursday, April 30, 2009

MATESO YA WATER BOARDING JUU YA WATUHUMIWA WA KIGAIDI RAIS BARAK HUSEIN OBAMA AFICHUWA SIRI ZA MR. BUSH




Water Boarding
Kutana na staili ya kinyama inayomlazimisha mateka/mfungwa au mtuhumiwa yoyote yule kutoa habari ambazo mtesaji anazihitaji. Mchezo huu wa hatari umekuwa ukifanywa na wanajeshi wa Kimarekani kwa wafungwa wa jela ya Guantanamo Bay huko Kuba (Cuba). Mheshimiwa Obama akaona isiwe tabu akatoa mafaili ya dondoo zote jinsi watu walivyoteswa kwa staili hii ya water boarding.
Yaani ni hivi: Unafungwa mikono na miguu kisha unafunikwa kichwa na kitambaa kisha unamwagiwa maji ili udhani kama unazama, zoezi hili laweza kufanywa kwa mda wowote ule ambao mtesaji anataka . Kisha chochote usemacho kinaweza tumika kama ushahidi wakati wa kesi! Ajabu!
Ila la ajabu na kweli ni jeshi la Marekani linapiga marufuku kumtesa mwanajeshi yoyote wa kimarekani anapokamatwa kivita! Je hii ni sawa?
Nadhani sasa ni sawia kuwa tunaishi kwa sheria za porini! Mwenye Nguvu ndie aliye sahihi! Kwani kibinadamu inajulikana kuwa usimtendee mwenzio usichotaka kutendewa wewe! Kwa ufupi waweza pata picha ya vita dhidi ya ugaidi ilivyo ya kidhalimu! Na tukiwa wapenda amani duniani tunapenda kuombea amani kwa dunia yote kwa ujumla!

No comments:

Post a Comment