KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, April 24, 2009

Raisi Mpya Mtarajiwa wa Afrika ya Kusini









Raisi mtarajiwa wa hapo Bondeni ndio huyo hapo, anaitwa Jacob zuma na kwa kweli hana mfano katika viongozi wa sasa, kwani jamaa kwa mila na kwa mambo ya kigeni vyote vyake. Ana wake lukuki na watoto kibao pia haijulikani nani atakuwa first lady wake. yaani vurugu tupu ila ukipendwa umependwa kwani nyota yake kwa wapiga kura wa Afrika ya kusini ni njema.Licha ya kuwa hana ya kutosha pia ana kashfa za kila aina kuanzia ngono mpaka kashfa za rushwa watu hawajaona mwengine zaidi yake.
Pongezi zetu ziende kwa watu wa kusini ya afrika na tunatumai atafanya mabadiliko ya maana kuondoa umaskini, kumpambana na maradhi ya ukimwi kupunguza uharifu uliokithiri maana kombe la dunia laja hapo mwakani wasije tutia aibu bure! pia kuondoa matabaka ya matajiri na maskini yaliokithiri. Mungu ibariki Afrika ya Kusini, Mungu ibariki Tanzania na Mungu ibariki Afrika nzima!

No comments:

Post a Comment