
Waandamanaji wanaomuunga mkono Alassane Ouattara
Tangazo hilo limekuja siku moja baada ya viongozi hao kushindwa kumshawishi Bw Laurent Gbagbo kuachia madaraka.
Mwenyekiti wa jumuiya ya kiuchumi ya Afrika Magharibi, Ecowas, ambaye pia ni rais wa Nigeria Goodluck Jonathan amesema mazungumzo bado yanaendelea.
Mshindi halali
Ecowas ina matumaini kuwa Bw Gbagbo atakubali kuachia ngazi na kumpisha Alassane Ouattara, ambaye anaaminika kuwa ndio mshindi halali wa uchaguzi.
Jumuiya hiyo imetishia kutumia nguvu iwapo atagoma kuondoka madarakani

Mwenyekiti wa Ecowas, Goodluck Jonathan
Kituo cha televisheni cha serikali kimetangaza kuwa mamilioni kadhaa ya wafanyakazi kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika wanaofanya shughuli zao nchini Ivory Coast, watakuwa hatarini iwapo nguvu za kijeshi zitatumika.
"Watarejea tena Januari 3, na watakaporudi, matokeo yake ndio yataamua hatua itakayochukuliwa," amesema Rais Jonathan.
"Panapotokea mzozo, panapokuwa na kutokuelewana, ni mazungumzo ndio yatatatua". amesema rais huyo wa Nigeria.
No comments:
Post a Comment