
Shirika hilo la UNHCR, linasema watu 2,000 wamerejeshwa mjini Mogadishu hivi karibuni na sasa maisha yao yako hatarini.
Mapigano yamekuwa yakiendelea kila siku katika mji huo wa Mogadishu kati ya wanamgambo wa kiislamu, na majeshi ya serikali yanayoungwa mkono na majeshi ya Umoja wa Afrika.

Baadhi ya maeneo hayo yako chini ya udhibiti wa wanamgambo wa al-Shabab, wanaohusishwa na kundi la kigaidi la al-Qaeda.
Wanamgambo wa Somalia
Wanamgambo wa Somalia
Serikali ya mpito ya Somalia, inadhibiti maeneo machache kati mji mkuu.

Mzozo huo umesababisha raia wengi wa Somalia kukimbilia usalama katika nchi zingine, na baadhi hata huwalipa wasafirishaji haramu wa binadamu ambao huwasaidi kuvuka Ghuba ya Aden na kuingia nchini Yemen.
Baada ya kufika Yemen, kuna wale ambao huamua kuingia nchini Saudi Arabia.
Mji mkuu wa Somalia Mogadishu, na maeneo mengine ya Kusini mwa Somalia yamekuwa katika hali mzozo kwa takariban miongo miwili.
No comments:
Post a Comment