
Inafahamika kuwa washukiwa hao wanne waliofikishwa mahakamani ni kutoka Tanzania, Somalia na Msumbiji.
Wote wanakabiliwa na mashataka ya kupanga njama ya mauaji na watafikishwa tena mahakamani Julai 14.
Watu wengine wawili waliokamatwa wakati wa msako mkuu wa polisi waliachiliwa baada ya mashtaka dhidi yao kufutwa.

Jenerali Nyamwasa anaamini serikali ya Rwanda ndiyo iliyohusika na jaribio la kumuua kwa risasi alipokuwa anaelekea nyumbani kwake mjini Johannesburg.
Serikali ya Rwanda inakanusha madai hayo kwa kusema hakuna sababu yoyote ya kumuua.
No comments:
Post a Comment