
Siphiwo Ntshebe, mwenye umri wa miaka 34, alilazwa hospitali mjini Port Elizabeth wiki iliyopita na alifariki dunia siku ya Jumaanne kwa mujibu wa kampuni inayouza nyimbo zake, Epic Records.
Alitazamiwa kuimba wimbo wake mpya "hope" katika sherehe za ufunguzi tarehe 11 mwezi wa Juni mjini Johannesburg. Wimbo huo una ujumbe maalum wa matumaini na imani uliotungwa na kutolewa na Bwana Mandela.
Mwaandishi wa BBC mjini Johannesburg, Pumza Fihlani anasema Ntshebe hakuwa maarufu sana nchini Afrika Kusini. Hata hivyo kwa yeye kutumbuiza katika sherehe za Kombe la Dunia kungempa fursa ya kujulikana zaidi nchini mwake
No comments:
Post a Comment