KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, May 28, 2010

Anyang'anywa Uraia Baada ya Kuoa Mke wa Pili


Mwanaume wa Uturuki ambaye alipata uraia wa Uswizi baada ya kuoa mwanamke wa Uswizi amenyang'anywa uraia baada ya kuoa mke wa pili kwa siri.
Mturuki huyo ambaye alipewa uraia wa Uswizi baada ya kumuoa mwanamke raia wa Uswizi, alinyang'anywa uraia na mahakama ya Uswizi jana baada ya kugundulika ana mke mwingine nyumbani kwao nchini Uturuki.

Mturuki huyo alikuwa akiishi maisha ya ndoa na mke wake wa Uswizi kwa miaka 26 lakini wakati huo huo alikuwa na mke mwingine nchini Uturuki ambaye amezaa naye watoto wawili, limeripoti shirika la habari la Uswizi, ATS.

Mwaka 2003 alipewa uraia wa Uswizi kutokana na ndoa yake na mwanamke huyo raia wa Uswizi.

Mke wake aligundua kuwa mumewe ameoa mke mwingine nchini Uturuki lakini alikaa kimya hadi hivi karibuni ikiwa imepita miaka mitano alipoamua kupeleka malalamiko wizara ya uhamiaji.

Wizara ya uhamiaji iliamua kumnyang'anya uraia Mturuki huyo ambaye aliamua kwenda mahakamani kukata rufaa.

Mahakama ya rufaa ya Uswizi imetoa uamuzi jana na kuamua Mturuki huyo anyang'anywe uraia na pasipoti ya Uswizi aliyopewa

No comments:

Post a Comment