KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Tuesday, December 8, 2009

Mgomo wa Daladala wazua kashehe Tz


Mgomo wa Daladala wazua kashehe Tz

Madereva wa mabasi zaidi ya tisini yanayotoa huduma ya usafiri katika jiji la Dar es Salaam, nchini Tanzania hii leo wanakabiliwa na hatua za kisheria kutokana na mgomo wa jana wa kusitisha huduma hiyo.
Mgomo huo unafuatia operesheni inayoendeshwa kwa pamoja na Mamlaka ya Usafiri wa Majini na Nchi Kavu, SUMATRA, jeshi la polisi na kampuni ya uwakala ya Majembe Auction Mart katika kukabiliana na makosa mbalimbali ya usalama barabarani.

Madereva wa mabasi hayo maarufu kama DALADALA wanasema faini za sasa ni kubwa mno ikilinganishwa na walivyokuwa wakitozwa kati ya dola ishirini na thelathini za Kimarekani kabla ya operesheni hiyo.

No comments:

Post a Comment