KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Monday, December 13, 2010

Remmy Ongala afariki dunia



MWANAMUZIKI mkongwe wa dansi nchini, Dkt. Remmy Ongala amefariki dunia leo jijini Dar es Salaam
Remmy ambaye alisifika kwa vibao vingi machachari ambavyo viliifundisha jamii kama wimbo wake maarufu wa "Kifo hakina huruma" na nyingine nyingi amefariki leo majira ya saa 9 usiku wa kuamkia leo nyumbani kwake Sinza jijini Dar es Salaam.

Remmy alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya kisukari kwa muda mrefu na hatima yake kuiaga dunia.

Habari zilizoifikia Nifahamishe.com alfajiri ya leo zilisema mwili wa marehemu umekwenda kuhifadhiwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili

Kwa habari zaidi kuhusiana na msiba huu endelea kusoma mtandao huu

No comments:

Post a Comment