KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Tuesday, December 14, 2010

Jela Miaka Mitano Kwa Kusoma Email ya Mkewe


Mwanaume mmoja wa nchini Marekani ambaye alifungua email ya mkewe na kugundua kuwa mkewe alikuwa akifanya mapenzi nje ya ndoa, anakabiliwa na kifungo cha miaka mitano jela.
Leon Walker mwenye umri wa miaka 33 mkazi wa Michigan nchini Marekani anakabiliwa na kifungo cha miaka mitano jela kwa kufungua na kusoma email za mkewe.

Leon alifungua email ya mkewe, Clara Walker, kwa kutumia kompyuta waliyokuwa wakiitumia pamoja nyumbani kwao.

Kwa kutumia password yake, Leon alifungua akaunti ya Gmail ya mkewe na alisoma email zake ambapo aligundua kuwa mkewe alikuwa akitembea nje ya ndoa.

Mkewe alikasirika baada ya siri hiyo kufichuka na aliamua kufungua kesi ya madai ya talaka ambapo pia alimfungulia Leon mashtaka ya kusoma email zake.

"Hii ni kesi ya kustaajabisha, hakuna sheria inayoweka wazi suala kama hili", alisema mwanasheria Frederick Lane.

Wachambuzi wa mambo wanasema kuwa hii ni mara ya kwanza sheria dhidi ya wizi wa nyaraka za siri kwenye masuala ya kibiashara inatumika kwenye masuala ya kifamilia.

Baadhi ya wanasheria wanasema kuwa huenda Leon akahukumiwa kwenda jela miaka mitano iwapo atapatikana na hatia ya kutumia password ya mkewe kusoma email zake.

Leon akiongea na waandishi wa habari alisema kuwa alichungulia email za mkewe ili aweze kujua chanzo cha mkewe kuwatelekeza watoto wao.

Kesi ya Leon itaanza kusikilizwa februari 7 mwakani.

No comments:

Post a Comment