KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, August 13, 2010

Slaa afanyiwa upasuaji wa mkono

MGOMBEA urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk Wilbroad Slaa, amelazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, baada ya kufanyiwa upasuaji wa mkono.
Alifanyiwa upasuaji huo jana, majira ya saa sita mchana kwa ajili ya merekebisho kwenye mkono alioumia kutokana na kuanguka bafuni alipokuwa mkoani MWanza.

HAta hivyo wanahabari waliotaka kwenda wodini na kutaka kujua hali yake inaendeleaje hawakuweza kuruhusiwa kuingia wodini kwa kile kilichoelezwa mgonjwa mwenyewe aliagiza wandishi wa habari wasiruhusiwe na taarifa kuhusiana na afya yake itatolewa na chama.


HAta hivyo msemaji wa chama hicho, Bw. Rwakatalwe alisema hali ya Dk Slaa inaendaela vizuri

No comments:

Post a Comment