KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Thursday, August 12, 2010

Mlipuko Rwanda : 7 wajeruhiwa


Polisi wamesema kuwa guruneti hilo lilirushiwa watu waliokusanyika katika kituo cha basi muda mfupi baada ya tume ya uchaguzi nchini humo kumtangaza Paul Kagame kama Rais kwa ushindi wa zaidi ya asilimia 93 ya kura.

Bado haijajulikana ni nani aliyehusika na shambulio hilo japo watu watatu wametiwa nguvuni na wanasaidia polisi na uchunguzi.

Hili ni shambulio la nne la magruneti katika miezi minne mjini Kigali na yanashukiwa kuhusika na uchaguzi mkuu wa nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment