KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Thursday, June 17, 2010

Ivory Coast yatoka sare na Ureno


Mshambuliaji wa Ureno Cristiano Ronaldo akibishana na Guy Demel wa Ivory Coast wakati wa mechi ya kundi G kati ya timu hizo, mjini Port Elizabeth.


Ivory Coast imetoka sare 0-0 na Ureno kwenye mechi ya kundi G la Kombe la dunia, katika uwanja wa Nelson Mandela Bay mjini Port Elizabeth.

Ivory Coast iliudhibiti mchezo lakini umaliziaji wa Gervinho na Salomon Kalou ukakosa kuzaa matunda.

Mshambuliaji wa Ivory Coast Didier Drogba aliingia katika kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Salomon Kalou baada ya shirikisho la soka duniani FIFA kumruhusu kufunga kifaa mkononi ili kulinda jeraha lake.

Hata hivyo kuingia kwa Drogba hakukufanikisha safu ya ufungaji, akibanwa na walinzi wa Ureno.

Awali katika mechi shuti la Cristiano Ronaldo liligonga mwamba.

Mechi ya Ivory Coast itakayofuata itakuwa dhidi ya Brazil siku ya Jumapili, kabla ya kumalizia michuano ya makundi dhidi ya Korea Kaskazini tarehe 25.

Mlinzi wa Ivory Coast Kolo Toure aliondoka uwanjani akichechemea baada ya kupata jeraha, na bado haijawa wazi ikiwa ataweza kushiriki michuano itakayofuata.

Refarii Jorge Larrianda aliwaonyesha kadi ya njano Cristiano Ronaldo na Guy Demel kwa kujibizana wakiambiana maneno yasiyokubalika.

Kundi la G linaelezewa na wengi kuwa kundi la 'kifo' , kwani mbali na Ureno na Ivory Coast, linajumuisha mabingwa mara tano wa kombe la dunia Brazil na Korea Kaskazini.

Vikosi
Ivory Coast: Boubacar Barry, Kolo Toure, Didier Zokora,Salomon Kalou (Didier Drogba, 66), Cheick Tiote, Gervinho(Abdul Keita, 82), Aruna Dindane, Siaka Tiene, Yaya Toure,Guy-Roland Demel, Emmanuel Eboue (Koffi Romaric, 89).

Ureno: Eduardo, Bruno Alves, Paulo Ferreira, Ricardo Carvalho, Cristiano Ronaldo, Pedro Mendes, Liedson, Danny (Simao Sabrosa, 55), Raul Meireles (Ruben Amorim, 85), Deco (Tiago, 62), Fabio Coentrao

No comments:

Post a Comment