KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, May 21, 2010

Aliyejaribu Kuulipua Ubalozi wa Marekani ni Mtoto Yatima

MWANAFUNZI Nassib [16] anayekabiliwa na tuhuma za kutaka kujaribu kulipua ubalozi wa Marekani jijini Dar es Salaam uchunguzi umebaini kuwa ni yatima anaishi na shangazi yake Kinondoni Moscow.
Habari hizo za uhakika kutoka ndani ya jeshi la polisi, zimebaini hilo na mwanafunzi huyo anaishi na shangazi yake aitwae Chiku Simba baada ya wazazi wake kufariki.

Imefahamika kuwa mtandao wa kigaidi wa Al Qaeda umekuwa ukitumia watoto yatima, watoto wa mitaani na wajane kuwatumia kufanya vitendo vya ugaidi.

Hata hivyo shangazi yake alishangaa kutokana na kitendo hicho na alisema ameshitushwa na taarifa alizozipata kutoka kwenye vyombo vya habari kwa kuwa mtoto wake huyo hakuwa na vitendo vya kihuni na vya ajabu na majirani walithibitisha kuwa mwanafunzi huyo alikuwa ni mkarimu na hakuwa mtu wa makundi na hana tabia ya kukaa vijiweni.

Hata hivyo kati ya wanafunzi nane waliokamatwa juzi na maafisa wa polisi waliounganishwa katika tuhuma hizo saba wameachiwa huru na mmoja ambaye ni Amani Thomas anaendelea kushikiliwa kwa kuwa yeye ndiye aliongozana na Nassib hadi katika jengo hilo la ubalozi .

No comments:

Post a Comment