KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, May 22, 2010

Ajali ya Ndege yaua yaua zaidi ya watu 150

Ajali ya Ndege yaua yaua zaidi ya watu 150.

Bangalore:

Watu wapatao 159 wamekufa baada ya ndege ya Shirika la Ndege la Air India aina ya Boeing 737-800 kupata ajali karibu na mji ulioko kusini mwa nchi hiyo wa Mangalore.

Televisheni nchini humo zimearifu kuwa watu saba wamenusurika katika ajali hiyo.



Shirika hilo la ndege limesema kwamba watu 166 walikuwemo ndani ya ndege hiyo wakati ilipopata ajali.

Hali ya hewa ya mawingu na upeo duni wa kuona inaripotiwa kuonekana wakati wa ajali hiyo. Na habari tulizozipata hivi punde zinasema kisanduku cha taarifa za kuongozea ndege kimepatikana.

No comments:

Post a Comment