KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Monday, August 31, 2009

TAWHIID

NENO TAWHIID NI UNGANISHO (KUFANYA KITU KIMOJA) NA LINATOKANA NA NENO LA KIARABU ‘WAHHADA’, LENYE MAANA YA KUUNGANISHA KUFANYA KITU KIMOJA. LAKINI NENO TAWHIID LINAPOTUMIKA KUMUELEZEA MWENYEZI MUNGU (YAANI TAWHIIDULLAH) LINA MAANA YA “KUMPWEKESHA MWENYEZI MUNGU” KATIKA KILA KITU, KWAMBA YEYE NI MMOJA NA UMOJA WAKE UNATOSHA KWA KILA KITU NA KILA JAMBO NA HANA MSHIRIKA.
KWA MUKTADHA HUO TAWHIID BASI NI IMANI KUWA MWENYEZI MUNGU NI MMOJA, HANA MSHIRIKA KATIKA UTAWALA NA MATENDO YAKE; HANA MFANO KATIKA ASILI YAKE WALA SIFA ZAKE; WALA HANA MPINZANI KATIKA UUNGU WAKE NA KUABUDIWA KWAKE. KWA HAKIKA TAWHIID NI DHANA YA KIMAPINDUZI INAYOLENGA KUMKOMBOA MWANADAMU KUTOKA KATIKA GIZA LA UJAHILI NA UKAFIRI KUMPELEKA KWENYE MWANGA. KUTOKANA NA MAELEZO HAYA NDIO TUNAPATA MAFUNGU MAKUU MATATU YA TAWHIID AMBAYO NI:
1. TAWHIIDIR – RUBUUBIYYA ( YAANI, KUMPWEKESHA MWENYEZI MUNGU KATIKA UTAWALA WAKE)
2. TWHIIDIL – ASMAA WASIFAAT ( YAANI, KUMPWEKESHA MWENYEZI MUNGU KATIKA MAJINA NA SIFA ZAKE)
3. TAWHIIDIL – IBAADAH ( YAANI, KUMPWEKESHA MWENYEZI MUNGU KATIKA KUABUDIWA)
VIPENGELE HIVI VITATU NDIVYO VINAVYOFANYA MSINGI WA SAYANSI YA TAWHIID.
VYOTE VITATU VINATEGEMEANA, NA KUCHA KIMOJAWAPO KUNAITIA DOSARI IMANI NZIMA YA TAWHIID. KIPENGEE KIMOJA TU KATIKA HIVYO KIKIKIUKWA BASI MTU HUZAMA KWENYE

WEMA + UJINGA = CHUKI




WEMA NI KITENDO CHA DHATI, KINACHOTENDWA NA MAPENZI YA MOYO WA NAFSI HUSIKA. SIKU ZOTE WEMA JAMBO JEMA HUTENDWA NA NAFSI KWA MAPENZI YA MOYO WAKE. ILI MTU AWEZE KUTENDA WEMA, NILAZIMA AJUWE SABABU, UMUHIMU, FAIDA NA HASARA ZA WEMA HUSIKA. WEMA UNATOKANA NA FAHAMU YA NAFSI JUU YA MSINGI WA MSAADA WA WEMA HUSIKA.

UJINGA NI KIFAA CHENYE UKOSEFU WA FAHAMU, KILICHOMO NDANI YA NAFSI YA MTU HUSIKA. UJINGA MSINGI WAKE NI KIZA KINENE. USICHOKIJUWA UNAHITAJI KUKIJUWA, ILI UWE NA FAHAMU JUU YAKE. ELIMU NDIO DAWA YA UJINGA, KWA SABABU UFUNGUO WA MLANGO WA UJINGA NI ELIMU, HUWEZI KUFUNGUWA MLANGO WOWOTE BILA UFUNGUO, NDIO MAANA TUNASEMA UKITAKA KUFUNGUWA MLANGO WA UJINGA, ILI UPATE MWANGA WA FAHAMU, UNAHITAJI ELIMU YA KUTOSHA.

CHUKI, NI KIFAA CHENYE SUMU NDANI YA NAFSI HUSIKA.
KIFAA HICHO (CHUKI) KINAKAA NDANI YA MOYO WA BINAADAMU. MOYO WA BINAADAMU SIKU ZOTE HUPENDA YULE ANAEUPENDA NA HUMCHUKIA YULE MWENYE KUUCHUKIA, NDIO MAANA NI RAHISI KWA KILA NAFSI KUWA NA ADUI AU RAFIKI. KUWA NA ADUI AU RAFIKI, KUNATOKANA KANA NA MATENDO NA MANENO YA KILA UPANDE (WEWE AU RAFIKI YAKO).
LICHA YA KUWA NAFSI NDIO YENYE MAAMUZI YA KUTENDA KAZI ZOTE ZA MWILI, LAKINI HUJIKUTA KATIKA KAZI NGUMU YA KULAZIMISHA MOYO WAKE, KUMPENDA ADUI WAKE. IKIWA NAFSI ITAJILAZIMISHA KUONGEA NA ADUI WAKE, KUNA DALILI AMBAZO MOYO WAKE(NAFSI) UTAZITOA ZA KUTORIDHIKA NA MATENDO NA MANENO VYA NAFSI ADUI.
• WEMA + UJINGA

WEMA TUMEONA KWAMBA NI MTINDO WENYE HEKIMA KATIKA MATENDO YAKE. NA MSINGI WAKE NI ELIMU, YENYE UKUTA BORA WA MATUMIZI YA MSAADA JUU YA MHITAJI.
UJINGA, TUMEONA KWAMBA MSINGI WAKE NI KIZA KINENE. HAKUNA MTU MWENYE KUPENDA AU KUPENDELEA KUISHI KATIKA KIZA KINENE, LA BALI KILA MTU ANAPENDA AISHI KWENYE MWANGA ILI AWEZE KUTENDA KAZI YAKE KWA UFANISI ZAIDI.
MTU MJINGA ANAPOKUTANA NA MTU MWEMA, HUPATA FARAJA YA MATENDO MAZURI NA MANENO YA BUSARA, LAKINI KWA UPANDE WA MTU MJINGA, HUWA KAMA KIPOFU KATIKA MTAZAMO WA MATENDO AU USIKIVU WA MANENO.

SIKUZOTE MTU MWEMA ANAJITAHIDI KULINDA HESHIMA YAKE, KATIKA MANENO(HUTUMIA MANENO YA BUSARA) NA MATENDO
( HUTUMIA MATENDO YENYE UNAFU KWA KILA UPANDE)

MTU MWEMA NJIA YAKE HUWA NI KUTAFUTA AMANI NA KUHAKIKISHA KWAMBA MLANGO WAKE WA UTULIVU UPO KATIKA NYANJA. BALI MTU MJINGA HAWEZI KUONA KWAMBA AMETENDEWA WEMA, BALI ATAONA KWAMBA MTU MWEMA ANAMNYIMA HAKI YAKE YA KUTENDA UJINGA.

MTU MJINGA HUWA NI MWEPESI WA KUPOTEZWA KWASABABU HAIJUI NJIA VIZURI, HATAKAMA ATAAMBIWA KWAMBA NJIA HIYO NDIO SAHIHI, ATAJIKUTA KATIKA MASHAKA, KWA SABABU HANA (MTU MJINGA) UFAHAMU WA ELIMU YA KUTOSHA JUU YA UMUHIMU, FAIDA, HASARA VYA JAMBO
(NJIA, UENDESHAJI WA GARI, UJENZI, MAPENZI, HURUMA, MSAADA….N.K) HUSIKA.

KUMBUKA YA KWAMBA SIKU ZOTE MWIZI HAAMINI KWAMBA KUNAMTU MWENYE UWEZO WA KUMLINDIA MALI YAKE BILA KUMUIBIA,SIKU ZOTE MWIZI HUAMINI KWAMBA KILA MTU NI MWIZI.




AU MZINZI HAAMINI KWAMBA KUNA WATU WEMA WASIOKUWA NA TABIA YA UZINZI,

AU MTU MWENYE UKOSEFU WA IMANI JUU YA KUWEPO MUNGU, HUWEZI KUMSAIDIA KATIKA JINA LA MWENYEZI MUNGU NA AKAKUBALI MSAADA WAKO.

YOTE HAYO, YANATOKANA NA UPUNGUFU WA ELIMU JUU YA KUJUWA FAIDA YA UMUHIMU, FAIDA NA HASARA VYA JAMBO ULIFANYALO.

MTU MINGA HUWA NI MWEPESI WA KUKUBALI KILA NENO NA KILA TENDO LIPITALO MBELE YAKE, BILA KUFANYA UCHAMBUZI WA KINA, KATIKA MSINGI WA MCHAKATO WA MANENO NA MATENDO HUSIKA. JAMBO HILO HUWA NILENYE KUANGAMIZA NAFSI YA MTU MJINGA NA KUSABABISHA MAUMIVU MAKALI NDANI YA MOYO WA YULE RAFIKI MWEMA.

IKIWA JAMBO HILO, LITAJITOKEZA KATIKA MSINGI WA KUSHAURIANA, NAKILA UPANDE UKLABAKI NA MSIMAMO WAKE, KATIKA UKUTA WA MANENO NA MATENDO, KITAKACHOFUATA NI KUTENGANA KWA WEMA NA UJINGA.

KUTENGANA KWA WEMA NA UJINGA, NI KAMA MTENGANO WA KIZA NA MWANGA. IKIWA MWANGA UNAHITAJIKA KATIKA MAENDELEO YA JAMII, KITAKACHOTOKEA NI KUATHIRIKA KIDOGO KWA ULE MWANGA HUSIKA, NA BAADAE MWANGA UTARUDI KWENYE KUNDI LA WATU WEMA, NA UTAPATA MAFANIKIYO MAZURI KUTOKA KATIKA KUNDI HUSIKA( KUNDI LA WATU WENYE KUHURUMIANA KATIKA MANENO NA MATENDO).

KWA UPANDE WA UJINGA, UTASHINDWA KUJITAMBUWA NA KUTAMBUWA UMUHIMU, FAIDA NA HASARA VYA KUMPOTEZA RAFIKI MKARIMU, AMBAYE NI YULE MTU MWEMA. MATOKEO YAKE UJINGA WAKE UTAOTA MIZIZI NA BAADAE ATAJIKUTA AKITUMIWA NA MAADUI WA YULE MTU MWEMA, KUMSHAMBULIA, KUMJERUHI…..KATIKA NJIA YENYE MISINGI YA MANENO NA VITENDO.





ITAKAPOFIKIA HATUWA HIYO,NDIO UTAONA KWAMBA MTU MWEMA, HAWEZI KUISHI NA MTU MJINGA KUTOKANA NA KIZA KINENE KILICHO TANDA NDANI YA MOYO WAKE(MTU MJINGA).

UKOSEFU WA BUSARA, UTAUFANYA MOYO WA YULE MTU MJINGA KUWA SILAHA YENYE MASHAMBULIZI DHIDI YA MTU MWEMA, BILA KUJALI FAIDA YAKE KATIKA JAMII. CHUKI ITACHUKUWA NAFASI KUBWA KWA UPANDE WA MTU MJINGA, NA KWA UPANDE WA MTU MWEMA,ATAJITAHIDI KUTUMIA UFAHAMU (ELIMU) WAKE ILI AWEZE KUEPUKA CHUKI YA MJINGA DHIDI YAKE.

IKIWA KIZA NA MWANGA, MATOKEO YAKE MSHINDI NI MWANGA, NDIO MAANA TUNASEMA WEMA NA UJINGA NI KAMA MWISHO WAKE NI CHUKI, LA KINI MLANGO WA MWISHO WAKE NI NINGELIJUWA.

YATIMA KATIKA MSINGI WA NJIA PANDA



YATIMA NI MTU GANI?

YATIMA NI MTU MWENYE UPUNGUFU WA MZAZI AU WAZAZI MAISHANI MWAKE.
ILI BINADAMU AWEZE KUWEPO NA KUTAMBULIKA KATIKA JAMII, LAZIMA AWE NA MAMA NA BABA KATIKA MSINGI WA KUZALIWA NA UKUTA WA MALEZI.
KUNA BAADHI YA WATU AMBAO WALIISHI BILA YA BABA WALA MAMA, NAO NI ADAMU NA HAWA. ADAMU NDIO BINAADAMU WA KWANZA KUUMBWA NA MWENYEZI MUNGU HAPA DUNIANI, NAFSI YAKE MWENYEZI MUNGU ALIIPA ZAWADI YA JINSIA YA KIUME NA HAWA AKAPEWA NAFASI YA PILI KATIKA UMBO LA
BINAADAMU, NAYE MWENYEZI MUNGU AKAMZAWADIA
JINSIA YA KIKE. HUO NDIO ULIOKUWA MWANZO WA MKE NA MME KUISHI NA KUPATA MTOTO AU WATOTO, KUPITIA NJIA YA MBEGU YA UHAI KATIKA MSINGI WA SHERIA YA NDOA NA UKUTA WA TENDO LA NDOA.
BINADAMU MWINGINE AMBAE ALIZALIWA BILA NDOA, TENDO LA NDOA, BABA, SHANGAZI, BAMDOGO AU
BAMKUBWA AU BABU KWA UPANDE WA BABA NI YESU
(NABII ISA).

UKIWATOA ADAMU, HAWA NA YESU, HAKUNA BINADAMU MWINGINE MWENYE UPUNGUFU WA MZAZI, KATIKA MSINGI WA CHANZO (KUZALIWA KUPITIA NJIA YA TENDO LA NDOA) CHAKE CHA MAISHA, WOTE WALIBAKI TUMETOKANA NA
TUNAZIDI KUTOKANA NA NASABA YA BABA NA MAMA.

BIBLIA KATIKA NJIA YA DINI FASI NA KUJALI YATIMA NA WAJANE

DINI SAFI NI IPI ?
DINI ILIYO SAFI, ISIYO NA TAKA MBELE ZA MUNGU BABA NI HII, KWENDA KUWATAZAMA YATIMA NA WAJANE KATIKA DHIKI PASIPO MAWAA.
( WARAKA WA YAKOBO 1 :27)

KWA MUJIBU WA BIBLIA, TUNAONA KWAMBA KILA NJIA INA JINA LAKE. KWAMFANO NJIA YA KUMJUA MWENYEZI MUNGU, INAITWA DINI. NA TUNAONA DINI KUWA NI NJIA YA WATU WENYE IMANI YA KUWEPO KWA MWENYEZI MUNGU, NA HUFANYA MATENDO YAO KATIKA MSINGI WA KUWAPENDA NA KUWA HURUMIA YATIMA. NA NDIO MAANA KATIKA RATIBA YA MAISHANI MWAO(WACHA MUNGU) JAMBO LA KWANZA NI KUMTAMBUA MWENYEZI MUNGU NA KUHAKIKISHA UPENDO WAO JUU YA MWENYEZI MUNGU, KWA KUTENDA MAPENZI YA MUNGU, KAMA KUWATEMBELEA MAYATIMA NA WAJANE.
KUWATEMBELEA YATIMA NA WAJANE, HAKUMANISHI KWAMBA LAZIMA UWE NAHELA AU MALI YA KUWAPA, LA MARANYINGINE WANAHITAJI KUKUONA NA KUZUNGUMZA NAWEWE MAZUNGUMZO YENYE MFUMO WA FARAJA NA MSINGI WA AMANI NA UKUTA WA UTULIVU BAINA YENU.

KILA MWANAMKE MWENYE MSINGI WA NDOA ,ANAWEZA KUWA MJANE BILA KUTEGEMEA NA KILA MTOTO MWENYE WAZAZI ANAWEZA KUWA YATIMA BILA KUTEGEMEA. NDIO MAANA NI JUKUMU LA KILA MWANAUME NA MWANAMKE WENYE MSINGI WA NDOA, WANATAKIWA WATOWE AU WAONESHE NAFASI YAO YA KWANZA KATIKA HARAKATI YA KUWASAIDIA WAJANE.
KWASABABU HAKUNA FAMILIA YENYE MKATABA WA KUEPUKA UJANE AU UYATIMA NDANI YAKE.

IKIWA HUTAKI KUWASAIDIA WATOTO WA YATIMA, KUMBUKA KWAMBA KESHO NA KESHO KUTWA UNAWEZA KUONDOKA (KUFA) NA UKAACHA MJANE AU WAJANE NA MZIGO WA WATOTO WA YATIMA DUNIANI.

IKIWA MLIKUWA BABA NA MAMA WENYE KUWAPENDA MAYATIMA NA KUWAJALI KATIKA MSINGI WA HISIA ZAO, MWENYEZI MUNGU ATAFANYA WAJANE AU MJANE WAKO KUNUSURIKA NA MATESO YA WANAWAKE NA WANAUME WASIO WAJALI WAJANE, HAPA DUNIANI.
NA IKIWA UMEACHA AU MMEACHA WATOTO WA YATIMA KATIKA MFUMO MZURI WA KUPENDA NA KUPENDWA KATIKA JAMII YA MAYATIMA, BASI ULINZI WA WATOTO WAKO, UTAKUWA NI MZURI NA WENYE ULINZI KATIKA JAMII.

NA MWENYEZI MUNGU ATAWANUSURU WATOTO WENU AU WAKO, KWASABABU NA WEWE AU NYINYI (BABA NA MAMA ) MLIWEZA KULINDA NA KUTETEA MASLAHI YA WATOTO YATIMA, BINDI MLIPOKUWA HAI.
TENDA MEMA NENDA ZAKO WENGI HUONA KAMA MANENO HAYO NI HADITHI, LAKINI MATENDO HAYO NI NUSRA JUU YA MTENDAJI NA NI AFYA YENYE MSINGI WA KUMBUKUMBU BORA KWA MPOKEAJI.
KUMBUKA YA KWAMBA KISASI KINALIPWA KWA MABAYA NA WEMA HULIPWA JUU YA MAZURI. IKIWA ULIMTENDEA MTU JAMBO ZURI, ATAKUOMBEA KWA MUNGU AKUPE BARAKA NA UTENDEWE MAZURI. HATA KAMA ULIMSAIDIA MTOTO YATIMA, ATAKUOMBEA BARAKA NA MAZURI KWA MWENYEZI MUNGU, KISHA UTAPATA ULINZI WA MUNGU, NA SIKU AMBAYO UTAKUWA NA MZIGO WA YATIMA KATIKA FAMILIA YAKO, BASI MWENYEZI MUNGU ATAKULIPA KUTOKANA NA ULE MSINGI BORA WA KUTENDEA MAZURI YATIMA , KWA HIVYO NAWE YATIMA WAKO WATALIPWA JUU YAYALE ULIYOYATANGULIZA MIKONO YAKO
(WEMA JUU YA YATIMA).



QURANI INASEMAJE ! KUHUSU YATIMA ?

MWENYEZI MUNGU ANASEMA HIVI » WALA MSIKARIBIE (MSIYAGUSE) MALI YA YATIMA, ISIPOKUWA KWA NJIA ILIYOBORA (KWA HAO MAYATIMA) MPAKA AFIKE BALEGHE YAKE(HUYO YATIMA AKABIDHIWE MWENYEWE). NA TIMIZENI AHADI, KWA HAKIKA AHADI ITAULIZWA «
(SIKU YA KIAMA)

(17 : 34)
KWA MUJIBU WA QURANI, TUNAONA KWAMBA KUNA WATU WENYE KUTUMIA MALI ZA WATOTO YATIMA, NA NDIO MAANA MWENYEZI MUNGU ALITOA TAHADHARI, JUU YAMATUMIZI MABAYA YA MALI ZA WATOTO YATIMA. KUNA WATU WENYE KUTUMIA VIFO AU KIFO CHA MZAZI KAMA MTAJI(DILI). BABA ANAPOKUFA, NDUGU AU WAZAZI WA MAREHEMU, HUANZA VIKAO VYA KUMNYANYASA MJANE ALIOACHWA NA MAREHEMU NA MARANYINGINE KUMDHULUMU HAKI YAKE YA MSINGI KATIKA MALI YA MUMEWE. KINACHOTOKEA NI UKOO HUSIKA KUMTIMUA MJANE YULE NA KUMNYANGANYA WATOTO, KATIKA MSINGI WA KUBAKI NA UTETEZI WA DHULMA YA MALI YA BABA YAO. KITENDO HICHO NI KITENDO AMBACHO NI KIBAYA NA HUTENGENEZA UHASABA BAINA YA MKE NA BABA, MAMA MKWE, MASHEMEJI, MAWIFI, WAJOMBA NA KUTENGANISHA UHUSIANO WA NDOA
(MKATABA WA MUUNGANO WA KOO MBILI).

MWANAMKE ANAPOTIMLIWA NA NDUGU WA MMEWE ATAJIKUTA AKIHANGAIKIA MAISHA YAKE NA AKIHANGAIKA KATIKA MSINGI WA KUKOSA MME, NA KUHANGAIKA KATIKA UKUTA WAKUKOSA MALEZI YA WANAE NA KUHANGAIKA KATIKA MLANGO WA KUDHULUMIWA MALI YAKE.

SI RAHISI KWA MWANAMKE HUYO, KUWA NA AKILI TIMAMU KATIKA JAMII. HUJIKUTA KATIKA HALI YA KUCHANGANYWA NA MZONGO WA MAWAZO NA KWA UPANDE MWINGINE MZIGO WA MATENDO YA KUTAFUTA RIZIKI. HALI HII, IMETENGENEZWA NA WATU AMBAO TAYARI WALIUNGANISHA NDOA (MUUNGANO WA KOO) HUSIKA, KATIKA MSINGI WA KICHEKO NA FURAHA, NA WAMEVUNJA MKATABA HUSIKA KATIKA CHUKI NA MAUMIVU YA KILA UPANDE, NA MWISHO WAKE WAKIPORA HAKI YA VIUNGO KATIKA VIUNGO VYA FAMILIA HUSIKA, NA KISHA WA KIONDOA UPENDO NA AMANI NA UTULIVU BAINA YA WATU HUSIKA KATIKA KOO HUSIKA.

KWA UPANDE WA WATOTO!!!!!!?

LICHA YA WATOTO, KUJIKUTA KATIKA JIA PANDA, KWA KUMPOTEZA BABA, KATIKA NJIA YA KIFO NA KUPOTEZA MAPENZI NA MALEZI YA MAMA KATIKA MAISHA YAO YA MAPITO, WATAJIKUTA WAKIWA NA UPUNGUFU WA AKILI(YAANI WATOTO WA YATIMA KATIKA HALI HII, HUJIKUTA WAKICHANGANYIKIWA KWA MZIGO WA MAWAZO NA VISHINDO VYA MAAMUZI KATIKA MSINGI WA MATENDO), KUTOKANA NA KUFIKIRI KIFO CHA BABA NA KUFIKIRI MTENGANO WAO NA MAMA MZAZI NA KUFIKIRI UPORAJI MALI ULIOTENDWA NA BABU, BIBI, BABA MKUBWA AU MDOGO, SHANGAZI……..KATIKA UKOO WAO.

KWA KWELI NJIA HII NI MBAYA NA NIJAMBO LA KUSIKITISHA KATIKA JAMII. WATU WENYE UPUNGUFU WA ELIMU JUU YA WATOTO YATIMA, WANAWEZA KUFIKIRI VIBAYA KUHUSU, UTENDAJI WAO WA KAZI NA MCHANGO WA MAONI YAO KATIKA JAMII. MTOTO YATIMA NA MTOTO MWENYE WAZAZI , KWANZA FIKIRA ZAO NI TOFAUTI. UTOFAUTI UNATOKANA NA MSAADA WA MAWAZO UNAOTOKANA NA BABA AU MAMA MAISHANI MWETU. UKOSEFU WA BABA AU MAMA, KIDOGO UNAWEZA KUTINGISHA KICHWA CHA YATIMA HUSIKA KWA MDA MFUPI KISHA AKAWEZA KURUDI KATIKA HALI YA KAWAIDA KIMATENDO NA KIFIKIRA. LAKINI UKOSEFU WA WAZAZI WOTE NI PIGO KUBWA, KAMA UGONJWA WA UKOMA KATIKA MOYO WA YATIMA HUSIKA. BABA NA MAMA, KILA MMOJA ANA UMUHIMU WAKE KATIKA MCHANGO WA MAWAZO NA MATENDO FULANI JUU YA WATOTO AU MTOTO WAO, BILA KUJALI JINSIA. MSAADA HUO, HUWA NI FARAJA KWA MTOTO HUSIKA, HATA KAMA BABA ATAKUWA NI MWEHU AU MLEVI, LAKINI KWENYE MOYO NA KATIKA JAMII UNAJULIKANA YA KWAMBA UNA MSINGI WA ULINZI, UMUHIMU, NA FAIDA YA KUWA NA BABA, NA KWA UPANDE WA MAMA NDIVYO ILIVYO.

JUU YA YULE MTOTO MWENYE UKOSEFU WA WAZAZI NA KUWA NA MSINGI WA DHULMA YA MALI YA BABA YAKE, HUWA KAMA MTU MWENYE UPUNGUFU AU UKOSEFU WA MAPENZI JUU YA KOO ZOTE MBILI(UPANDE WA BABA NA UPANDE WA MAMA) WOTE HUONEKANA KWAKE KAMA WATU WANAFIKI, WALIOSHINDWA KURUDISHA HAKI YA WAZAZI MKONONI MWAKE, NA MWISHOWE KUNDI FULANI LIKAJILIMBIKIZA MALI ZA WAZAZI WAKE, KATIKA JINA LA KUOKOA MALI ZA NDUGU YAO, BILA KUJALI MBEGU YENYE KUTOKANA NA MGONGO WA NDUGU YAO, HIYO ITAKUWA NI NJIA YA KUJENGWA VITA YA MAWAZO NA MATENDO NA KUONDOA RAHA YA UJOMBA, SHANGAZI, BABA MKUBWA AU MDOGO, MJOMBA, BIBI AU BABU.

MAMBO HAYA YAPO NA TUNAYASHUHUDIA KILA KUKICHA KATIA RUNINGA, MAGAZETI ……..N.K.

UKIMWONA MTOTO YATIMA AMEKAA MWENYEWE JUWA YA KWAMBA HANA RAHA MAISHANI MWAKE, WALA USIMKEMEE, ANACHOKIHITAJI NI MATIBABU YENYE MZINGO WA UPUNGUFU WA UPENDO NA KIZINGITI CHA KUPATA HAKI ZENYE UKUTA WA MALEZI BORA NA MLANGO WA ELIMU BORA KATIKA JAMII.

Ndugu kuchukuwa mali ya yatima au yatima katika jina la utunzaji bora

KUNA BAADHI YA NDUGU AMBAO WANAJIVIKA NGOZI YA KONDOO KUMBE NI MBWA MWITU NDANI YA NYOYO ZAO. WATU BHAWA HUTAMBULIKA KWA MANENO MAZURI NA MATENDO YENYE KWENDA KINYUME NA MISEMO YAO, KWA KIFUPI WATU HAO NI WANAFIKI.

UTAWAKUTA WAKICHUKUWA JUKUMU LA KUWALEA WA TOTO YA TIMA KATIKA JINA LA KUWAPA MALEZI BORA NA KUWALINDA KATIKA MSINGI WA HAKI, LAKINI MIOYONI MWAO WANA LENGO LINGINE KABISA.





MALENGO KATIKA MALEZI YAKO AINA KUU TATU

1. LENGO LA KUTUMIA (KUDHULUMU) MALI YA YATIMA HUSIKA.
WATU HAO, HUCHUKUWA JUKUMU LA KUWALEA WATOTO HUSIKA, KATIKA MSINGI BORA WA MALEZI NA KUMBE LENGO LAO KUU NI KUTUMIA MALI ZAO KATIKA MAHITAJI YAO BINAFSI. MLEZI HUTUMIA MALI YA MTOTO YA TIMA BILA RIDHA YAKE WA LA MTOTO KUJUWA. KINACHOFANYIKA, NI KUTUMIA ILE MALI KWA JINA LA KULA WOTE (KUTUMIA MALI YA YATIMA KATIKA MATUMIZI YA FAMILIA HUSIKA AU UKOO HUSIKA, BILA RIDHA YA YATIMA (MMILIKI) HUSIKA KUJUWA, HATA KAMA ATAJUWA ATAJIKUTA HANA UWEZO WA KUZUIA MALI HUSIKA KUTUMIWA. WATU HAWA NI WATU WENYE UPUNGUFU AU UKOSEFU WA HURUMA JUU YA YATIMA. NDIO MAANA UKITAKA KUCHUKUWA YATIMA NA KUMLEA UWE NA UHAKIKA, KUTOKA MOYONI MWAKO KWAMBA UTAKUWA NA ULINZI WA KUMLINDA NA KULINDA MALI YAKE KATIKA JINA LA KWELI. MATOKEO YAKE YULE MTOTO ATAJIKUTA, KATIKJA NJIA PANDA NA KUTESWA PINDI MALI YAKE ITAKAPO KWISHA. MALI YA YATIMA ITAKAPOKWISHA, FAMILIA HUSIKA ITAANZA KUMWONA YULE MTOTO KAMA MTU MWENYE KUFIRISI FAMILIA HUSIKA, NA KITAKACHOTOKEA JUU YA MTOTO HUYO NI KUMTENGENEZEA MBINU ZA KUMWANGAMIZA KIFIKIRA AU KUMFUKUZA BILA JAMII KUTAMBUWA SIRI ILIOKO BAINA YAO(MTOTO YATIMA NA WALEZI).
MBINU ZIKO NYINGI ATAITWA MWIZI, MALAYA, MKOSA ADABU, MTU MNAFIKI, KAMPENDA MMEWANGU, ALITAKA KUMBAKA MKEWANGU AU MWANANGU AU KANIIBIA KIASI FULANI CHA PESA……N.K.

KITAKACHOTOKEA JAMII ITAMWONA MTOTO HUSIKA, HANA ADABU NA ITAOGOPA KUMKARIBISHA MAJUMBANI MWAO. NJIA HII NI NJIA IPO NA INATUMIWA NA KOO NA FAMILIA NYINGI MAISHANI MWETU.

2) LENGO LA KUMCHUKUWA MTOTO YATIMA ILI KUMFANYA MFANYAKAZI AU MTUMWA


KUNA BAADHI YA FAMILIA ZINAZOCHUKUWA WATOTO YATIMA, KWA LENGO LAKUWATUMIA, KAMA WAFANYAKAZI WA NYUMBANI. WATU HAWA HUWA NI WENYE MANENO MAZURI MBELE ZA WATU LAKINI MIOYO YAO INA KUTU KATIKA NJIA YA MALEZI YA WATOTO YATIMA.

KWANZA ANAPOCHUKULIWA MTOTO HUYO, HUWA NI MWENYE KUHISI FURAHA NA FARAJA MOYONI MWAKE(MTOTO YATIMA), LAKINI MATOKEO YAKE HUJIKUTA KATIKA DIMBI LA KINYUMBE CHA FIKIRA. MWANZO HUDHANI KWAMBA MANENO YA MUONGEAJI NIYA KWELI KATIKA UTENDAJI, MARA HUONA MABADILIKO KATIKA MSINGI WA MAUMIVU NA CHUKI JUU YAKE. KILA KAZI NGUMU HUPEWA YEYE, HUWA NI MWENYE KUAMKA WA KWANZA NA KULA NA KULALA HUWA NIWA MWISHO. MAUMIVU HAYA, KWA KWELI NI MAUMIVU YENYE KUMFANYA MTOTO YATIMA AKOSE RAHA YA UTULIVU NA AMANI MAISHANI MWAKE. SI KAZI NGUMU TU HUYO MTOTO ATAPEWA, LA! BALI HUJIKUTA KATIKA KIPIGO NA MATUSI NA MAARANYINGINE MANENO YA KEJERI. HALI HIYO HUMFANYA MTOTO HUSIKA AANZE KUWAZA UMUHIMU, FAIDA NA HASARA YA KUWA NA WAZAZI NA MARANYINGINE HUJIKUTA KATIKA KUPOOZA AU KUKOSEKANA KWA MAPENZI JUU YA WALEZI WAKE.
MLEZI MWENYE ROHO MBAYA KAMA HII, HAWEZI KUMPA MTOTO YATIMA HATA FURSA YA KUPELEKWA SHULENI AU KUJISOMEA. NA ATAKAPO MPELEKA MTOTO HUYO SHULE, BASI ATAMPANGI YA RATIBA YA KAZI ZA NYUMBANI BILA KUJALI MDA WAKE WA KUPUMZIKA AU KUJISOMEA. MWISHO WAKE MTOTO HUYO ATAKUWA NI MWENYE MAWAZO AU MZIGO MKUBWA WA MAWAZO NA ATAJIKUTA AKISHINDWA KUSOMA VIZURI NA MARANYINGINE KUFAULU.
UKIANGALIA WATOTO WENGI WA YATIMA WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA KAMA HAYA, WENGI WA MEMALIZA DARASA LA SABA NA WENGINE WAMESHINDWA KUMALIZA ELIMU YA JUU. SIKUSEMA KWAMBA WATOTO HAO WAMEKOSA ADA L! BALI WALICHO KIKOSA NI UHURI AU UKOSEFU WA UTULVU NA AMANI NDANI YA NAFSI ZAO. NA MWISHO WAKE WALEZI HAO WABAYA HUPANDISHA BENDERA NA KUTAMKA KATIKA JAMII, KWAMBA MTOTO AMESHINDIKANA, HATAKI SHULE, NI RAHISI SANA KWA JAMII KUKUBALI MANENO YA MLEZI HUYO MBAYA , KUTOKANA NA KUWA NA MANENO MAZURI NA KUCHUKUWA MAAMUZI YA MATENDO YENYE SIRI YA NDANI YA NAFSI YAKE. MTOTO HUSIKA ATAONEKANA KAMA MTU MWENYE BAHATI LAKINI ANAICHEZEA NA MARANYINGINE ATALAUMIWA NA JAMII KWA KUTOTUMIA NAFASI YAKE YA BAHATI VIZURI. KAMA TUNAVYO JUWA SIRI YA MTUNGI AIJUWAE VIZURI NI KATA YAKE AU SIRI YA NDOA AIJUWAE VIZURI NI BABA NA MAMA AU WENYE NDOA. NDIO MAANA MLEZI HUYO HUTUMIA NGUVU YAKE YA MANENO KUANGAMIZA UTU NA NAFASI YA MALEZI NA ELIMU BORA YA MTOTO HUSIKA, KATIKA JINA LA WEMA. HAKUNA WEMA WENYE MATESO, WEMA WENYE MATESO MWISHO WAKE NI KISASI. NA TUNAJUWA YA KWAMBA KISASI NI MALIPO YA UBAYA WA NAFSI. IKIWA UMEAMUWA KUTENDA WEMA, BASI KUWA MFANO MZURI WA KUTENDA ULICHO KINENA NA UWE MVUMILIVU KATIKA UENDESHAJI, KWASABABU HAKUNA BINADAMU MWENYE UKOSEFU WA KASORO, HATA WEWE UNAKOSEA.

USITOWE VISINGIZIO VYA UONGO KWASABABU, MWENYE MPINI NI WEWE LEO KWAKO KESHO KWAKE, SIJUI ITAKUWAJE MKIKUMBANA NA ULIEMTESA KATIKA MSINGI WA KUHITAJI MSAADA WAKE. TENDA WEMA NENDA ZAKO NA IKIWA HUWEZI, USIJIPE JUKUMU HILO KWASABABU HULIWEZI. IKIWA NI MFANYAKAZI MTAFUTE KWA JINA LA AJIRA SIO KWAJINA LA MALEZI BORA.


3) KUANGAMIZA ELIMU NA UWEZO WA YATIMA.

KUNA BAADHI YA WATU KATIKA UKOO AU KOO, WAO HUWA NA ROHO ZENYE MSINGI WA CHUKI, WIVU, FITINA, LAWAMA, LAANA…… JUU YAKILA MTU AU FAMILIA YENYE MAFANIKIO KATIKA MFUMO WA MALI, PESA, ELIMU, CHEO, HESHIMA…………N.K.
WATU HAO NI WABAYA, WALA SIOWATU WAKUPEWA MTOTO WA YATIMA KWALENGO LA KUMLEA, KWASABABU HAWANA, MOYO WA MSAADA, BALI WANAHITAJI KILA JAMBO ZURI LIWE LA KWAO, BILA KUJALI UMUHIMU, FAIDA NA HASARA VYA JAMBO HUSIKA.

MTU HUYO, HUWA NA KAULI NZURI KATIKA UKOO AU FAMILIA HUSIKA. HUWA NI MTU MWENYE MAZUNGUMZO MAZURI YA ULIMI NA MSINGI WENYE TOFAUTI, KATIKA MATENDO YAKE.

KUNA BAADHI YA FAMILIA AMBAZO HUAMINI KWAMBA, NDIZO ZENYE KUSTAHIKI HESHIMA YA MALI, PESA, ELIMU, CHEO……N.K, WATU HAO, HUWA NI MARACHACHE KUWA NA MOYO WAKUWEZA KUSAIDIA, BAADHI YA WANACHAMA WA UKOO WAO, ILI WAWEZE KUPATA, ELIMU, MALI, PESA, CHEO, HESHIMA…….N.K, KUTOKANA NA NYOYO ZAO KUJAWA NA WIVU, FITINA, LAWAMA, HUSUDA, LAANA, CHUKI……..N.K.

WATU HAWA WATAKAPOMCHGUKUWA MTOTO WA YATIMA, ATAKUWA NI MWENYE KUFURAHI NA MWENYE KUHISI KUPATA NAFUU MAISHANI MWAKE. LAKINI MATOKEO YAKE MTOTO HUYO WA YATIMA ATAJIKUTA KATIKA, ULINZI WA MALI NA MARANYINGINE KUPEWA MAJUKUMU YA KIBIASHARA. MTOTO WA YATIMA ANAPOPEWA BIASHARA, HUJIHISI KUWA NA NAFUU KUBWA MAISHANI MWAKE, KWASABABU ATAHISI KWAMBA TAYARI ANA UHAKIKA WA KUISHI BILA TAABU, LICHA YA WAZAZI WAKE KUFARIKI. ITAKUWA NGUMU JUU YA MTOTO HUYO YATIMA, KUGUNDUWA KWAMBA NI MCHEZO WA KUMWANGAMIZA KIELIMU NA KIMAFANIKIO ZAIDI, BALI ATAONA HAKUNA FAMILIA YENYE MAPENZI YA MAANA KAMA HIYO, AMBAYO IMEWEZA KUMPA AJIRA NA KUMPA NAFASI YA TWISHENI.

BINAADAMU WANA MBINU NYINGI ZA KUANGAMIZA ELIMU NA HESHIMA YA MTU, NA HUJUWA VIZURI YA KWAMBA UKIMWANZISHIA BINAADAMU MAISHA MAZURI NA YENYE KIPATO, ATAKUWA RADHI KUACHA HATA SHULE, KUMBUKA YA KWAMBA HUYO MTOTO HANA WAZAZI WA KUMSHAURI, NA WALE NDUGU WALIOBAKI HAWAWEZI KUMKEMEA AU KUMKEMEA MLEZI WAKE, KWASABABU ASILIMIA KUBWA YA UKOO, HUPELEKA PALE(KWA MLEZI MWENYE MALI, PESA, CHEO……N.K) MALALAMIKO YAO YA NJAA NA SHIDA NYINGINE NDOGO NDOGO, HUMUONA HUYO MLEZI NI MKOMBOZI WA UKOO HUSIKA, NA WENGI KATIKA UKOO HUSIKA , WANATAJA TABIA ZAKE MBAYA KWA KUJIFICHA (KWA SIRI) NA YULE MWENYE KUTHUBUTU, KUULIZA KUHUSU HAKI YENYE MSINGI BORA WA FAHAMU (HAKI YA ELIMU) NA KUHOJI KUFANYA BIASHARA VYA YULE MTOTO WA YATIMA, KABLA HAJAFIKIA UMRI AU KUWA NA UWEZO THABITI WA KUKABILIANA NA AJIRA HUSIKA.

ATAKUMBANA NA UPINZANI WA CHUKI, VITISHO VYA KUSITISHA MISASADA(CHAKULA,CHUMVI, 5000 AU 2000 ELF, NGUO, MCHANGO WA HARUSI YA MWANAE, SALAMU YA TAJIRI…..N.K).

NJIA HII, YAKUMPA MTOTO YATIMA NAFASI YA KIBIASHARA, KABLA HAJAFUDHU(KUMALIZA) MASOMO YENYE MSINGI WA ELIMU YA CHINI, KATI NA YA JUU KABISA, NI NJIA YA KUANGAMIZA ELIMU YA UTAMBUZI WA MENGI MAISHANI, UTAJIRI WA AJIRA BORA KATIKA MASHIRIKA MBALIMBALI, HESHIMA YA CHEO CHENYE KUHITAJI ELIMU FULANI……………………….N.K.

• FAMILIA YENYE TABIA HII, MARANYINGI UNAKUTA NIYENYE WAPENZI WACHACHE KATIKA UKOO HUSIKA. VILEVILE FAMILIA HII, HUWA NIYENYE UBAGUZI BAINA YA MATAJIRI NA MASIKINI, NA BAINA YA WATU WENYE ELIMU KUBWA NA MASIKINI WA ELIMU.
• FAMILIA HII HUWA NIYENYE KUHAKIKISHA KWAMBA INAANGAMIZA, KILA MTU MWENYE KUTAKA KUCHIPUWA NDANI YA UKOO, AKIWA NA MSINGI WA UTUKUFU WA ELKIMU NA MSINGI WA KUTENGENEZA MAZINGIRA YA AJIRA BORA, KATIKA JAMII.







MTAZAMO WA JAMII JUU YA YATIMA UKOJE?


KWANZA JAMII, IMEJIKUTA KATIKA MTIHANI MGUMU, WA MATUMIZI YA DARUBINI YAKE JUU YA WATOTO YATIMA.

HAKUNA MTU MWENYE UWEZO WA KUEPUKA UYATIMA AU KUKOSA YATIMA KATIKA UKOO WAKE. JAMBO HILI LAZIMA LIWE ALAMA YENYE KUBEBA ELIMU YA MSAADA JUU YA
WATOTO WA YATIMA.

LAKINI JAMBO LA KUSHANGAZA KATIKA JAMII, NI KUWA MSINGI WA MATUNZO BORA YA WATOTO WA YATIMA, UMEACHIWA WAFADHILI WA KIGENI NA MARANYINGINE, JUKUMU HILO LIMEELEKEZWA KATIKA VITUO VYA MALEZI.

BAADHI YA WATU KATIKA JAMII WANAJITOLEA MALI, PESA, ELIMU NA MDA, KATIKA HARAKATI YA KUWASAIDIA WATOTO HAO WA YATIMA.

KUNA WATU WENGINE AMBAO, HUCHUKUWA MTOTO AU WATOTO WA YATIMA NA KUCHUKUWA JUKUMU LENYE MSINGI WA MALEZI BORA NA UKUTA WA AMANI NA UTULIVU.

NA KUNA BAADHI YA WATU, AMBAO HUONA JUKUMU LA KUMLEA MTOTO WA NDUGU, JAMAA NA RAFIKI KUWA NI KERO. NA MARANYINGINE NDUGU (BABA MDOGOAU MKUBWA, SHANGAZI, WAJOMBA, WAKE ZAO AU WAUME WAO………N.K) HUCHUKUWA KASORO YA MAREHEMU(BABA AU MAMA) NA KUZIFANYA SABABU YA KUCHUKIA WATOTO HUSIKA.
NA MARANYINGINE WATOTO YATIMA HUJIKUTA KATIKA NJIA PANDA, PALE WANAPOKABILIWA NA WAKATI MGUMU WA KIFO CHA MAMA. MAMA MZAZI NI KIUNGO CHENYE MSINGI WA MALEZI BORA NA UKUTA WA HURUMA JUU YA MWANAE. NDIO MAANA MARANYINGI, KIFO CHA MAMA MZAZI KINAUMIZA SANA ZAIDI YA KIFO CHA BABA MZAZI.

ASILIMIA KUBWA SANA YA WATOTO WA MTAANI, AMBAO NI YATIMA, WAMEFIWA NA MAMAZAO. SABABU KUBWA INAJITOKEZA ,KUTOKA KWA UPANDE WA BABA.
MAMA MZAZI ANAPOKUFA(KUONDOKWA NA ROHO), ASILIMIA KUBWA YA MAISHA YA MTOTO AU WATOTO WAKE, INATETEMEKA KWA KISHINDO KIKUBWA. MTOTO HUWA NI MWENYE KUPOTEZA MSINGI WA HURUMA NA UKUTA WA MWONGOZO KUTOKA KWA MZAZI WAKE WA KIKE(MAMA). NA NDIO MAANA MARANYINGI UTAMKUTA AU UTAWAKUTA WATOTO YATIMA, WAKIPENDA KUKAA,SEHEMU TULIVU NA MARANYINGINE WAKILIA.
MACHOZI YA MTOTO YATIMA YANATOKANA NA MACHUNGU YA NAFSI YAKE. MACHUNGU YA NAFSI YANATOKANA NA UPUNGUFU AU UKOSEFU WA MSINGI BORA WA MALEZI NA NGUZO YA HURUMA JUU YAO (WATOTO YATIMA).

KIFO CHA MAMA NIMSIBA MKUBWA JUU YA YATIMA HUSIKA, KWASABABU, MAMA ANAPOKUFA NIRAHISI SANA MWANAUME, KUOA MWANAMKE MWINGINE NA KUMSAHAU YULE ALIYETANGULIA MBELE YA HAKI
(KILA NAFSI LAZIMA ITAKUFA).
BAADHI YA WANAUME HUJIKUTA WA KIKUMBWA NA MAJUKUMU MENGI YA KUTAFUTA RIZIKI, NA MARANYINGINE WAKIJIKUTA WA KITOA MAJUKUMU YAO YA NYUMBANI, KAFARA KWA WAKE ZAO AU WALEZI.

KWANINI TUNASEMA MWANAUME ANATOA MAJUKUMU YAKE YA NYUMBANI KAFARA ?

KWASABABU NI MDA MFUPI SANA, MWANAUME
(BABA MWENYE FAMILIA), ANAOWEZA KUUTUMIA NYUMBANI MWAKE NA AKAUTUMIA KATIKA MSINGI WA KUONGOZA NA KUPATANISHA FAMILIA YAKE, KATIKA UKUTA WA HAKI. UTAMKUTA MTOTO ANA MATATIZO NA MAMA YAKE WA KAMBO, LAKINI NJIA INAYOTUMIKA KUTENGENEZA, KUENDESHA NA KUTATUWA TATIZO HUSIKA, HALIMUHUSU BABA MWENYE FAMILIA. UTAKUTA WATU WENYE MATATIZO, NDIO BABA ANAWAACHIA JUKUMU LA KUMALIZA TATIZO HUSIKA.
KUMBUKA KWAMBA MTOTO SIKU ZOTE NI MTOTO, LAKINI MKE ANA NAFASI YAKE NZURI NA YENYE CHEO CHAKUMWEZESHA KUFICHA, KUANGAMIZA NA KUMFUTA MTOTO YATIMA NDANI YA NYUMBA HUSIKA, BILA KUJALI YA KWAMBA NYUMBA HIYO ILIJENGWA KWA USHIRIKIANO WA MAREHEMU MAMA YAKE NA BABA YAKE.

KWA MTAZAMO WA HARAKA, LAZIMA TUJIULIZE KUHUSU CHANZO CHA MAPAMBANO BAINA YA WATOTO YATIMA NA MAMA WA KAMBO !!!!?

KWANZA KIFO CHA MWANAMKE, KINAMSTUWA MME WAKE, KUTOKANA NA MAZINGIRA YA MAISHA. LAKINI KIFO CHA CHA MAMA (MAMA WA FAMILIA) HUWA NI ALAMA YA MSIBA NA YENYE KUATHIRI KWA KIASI FULANI FIKRA(MTAZAMO) YA YATIMA HUSIKA KWA MDA FULANI.

SASA UHARAKA WA BABA KUOA, UNAWEZA UKAATHIRI WATOTO WAKE, IKIWA HAJAWAWEKA, KATIKA HALI YA MAANDALIZI YA KUISHI NA MAMA WA KAMBO. BABA ANATAKIWA KWANZA KUWAFARIJI WATOTO WAKE KATIKA MSINGI WA HURUMA NA MALEZI BORA NA PILI KUWAPA MAANDALIZI KATIKA MSINGI WA FURSA YA UHURU WA KUTOA MAONI NA KUPEWA MAJIBU, BILA UKUTA WA KHOFU NA UBABE.
TATU BABA LAZIMA ANAPOMUOA MWANAMKE WA PILI NA AKIWA NA WATOTO YATIMA(YATIMA KWA UPANDE WA MAMA), LAZIMA AWE MUAZI BAINA YA MKE MPYA NA WATOTO WAKE.
NA LINAPOTOKEA TATIZO BAINA YAO, BASI AWE NIMWENYE KUSIKILIZA KILA UPANDE NA KUJENGA MSINGI WA UTULIVU NA UKUTA WA HAKI BAINA YA NYOYO ZOTE ZENYE CHUKI AU KUTAFAUTIANA KIMANENO NA MATENDO.







KUMBUKA YA KWAMBA HAKUNA MTU ALIYEKAMILIKA MAISHANI MWAKE, WATU TUNACHUKIA NA KUPENDA. NA KILA UPENDO AU CHUKI, NI LAZIMA KILA KIMOJA KIWE NA SABABU.
NYOYO ZIMEUMBWA KWA KUCHUKIA WALE WENYE KUZICHUKIA NA KUWAPENDA WALE WENYE KUZIPENDA.

NDIO MAANA TATIZO LA NDANI YA NYUMBA, BAINA YA MAMA WA KAMBO NA WATOTO YA TIMA, LINAWEZA KUTOKANA NA MATENDO NA MANENO YENYE UKOSEFU AU UPUNGUFU WA MSINGI WA UPOLE NA UPENDO.
SIKU ZOTE VURU HUANZISHWA NA UPUNGUFU AU UKOSEFU WA HAKI, BAINA YA NAFSI (UKOO, FAMILIA,NDUGU,JAMAA NA MARAFIKI) HUSIKA, KATIKA MZOZO HUSIKA.

NA UTAKUTA MAMA WAKAMBO, MARANYINGINE HAJALI, MAUMIVU (HISIA ZA WALE WATOTO WA YATIMA) YA WALE WATOTO, NA KUTUMIA MANENO NA AMRI ZA KIBABE NA MARANYINGINE AKIWAPA ADHABU YA KIPIGO CHA MAANA NA MARANYINGINE AKIWAPIGA KIPIGO CHENYE MSINGI WA NJAA NA KIU NA MAVAZI DUNI NA MARANYINGINE WAKINYIMWA HAKI YA ELIMU. HII INAWEZA KUWA NJIA MOJA WAPO YA KUJENGA MAZINGIRA YA CHUKI NA VITA NDANI YA NYUMBA AU FAMILIA HUSIKA.

BABA SIRAHISI KUJUWA HISIA NA MAUMIVU YA MTOTO AU WATOTO WAKE, KUTOKANA NA KUWA NA MDA MFUPI SANA WA KUKAA NYUMBANI, MARANYINGINE MWANAMKE ANAWEZA KUFICHA SIRI YA MAPAMBANO BAINA YAKE NA WATOTO NDANI YA NYUMBA, KWA KUPITIA NJIA YA KUMDHIBITI MME WAKE KATIKA MDA WA KUWEPO NYUMBANI. MWANAMKE ANAWEZA KUMSHAWISHI MME WAKE KUANGALIA MUVI(PICHA) FULANI AU KWENDA KUMTEMBELEA FULANI AU KUMDHIBITIA MUME WAKE CHUMBANI, ILIMRADI ASIMPE NAFASI YA KUKAA NA KUANZA KUJADILIANA NA WATOTO WAKE, KUHUSU HISIA NA MTAZAMO WA MAISHA YAO.
HIZO NI BAADHI YA NJIA AMBAZO BAADHI YA WANAWAKE WANAZITUMIA, KATIKA KUFICHA MAKUCHA YAO.SIKU ZOTE MWANAMKE ANAPOTAKA KUANGAMIZA AU KUTENGENEZA CHUKI BAINA YA MUME NA BABA, MAMA, NDUGU, JAMAA NA MARAFIKI, LAZIMA KWANZA AJUWE UDHAIFU WA MUME, ILI AWEZE KUPATA NAFASI NZURI YA KUMDHIBITI BILA KUFURUKUTA. KWA UPNDE WA MIKAKATI YA MWANAMKE MWENYE MOYO WA UPUNGUFU WA UPENDO JUU YA UKOO WA MWANAUME, ANAPOKUWA NAMPANGO WAKE, WAKULIPUWA (KUWAFANYIA UBAYA AU KUWAFUTA KATIKA DAFTARI LA UPENDO LA MME WAKE NA KULIANDIKA KATIKA DAFTARI LA CHUKI LA FAMILIA NZIMA NA KUPIGA MUHURI WA VURUGU KATIKA UKOO AU KOO HUSIKA. KIUNGANISHI CHA KOO HUSIKA NI NDOA, NA KASORO YA NDOA NDIO KASORO YA FAMILIA HUSIKA. KASORO YA FAMILIA INAKUWA NI KASORO YA MUUNGANO WOTE WA KOO HUSIKA.

KWA KIFUPI WANA WAKE, NI VIUMBE WENYE HURUMA SANA. LAKINI LINAPOFIKIA SWALA LA KUMLEA MTOTO WA MWENZIWE, PANATOKEA MSHIKEMSHIKE YA AJABU NA KUANZA KUJIJENGEA MAZINGIRA YA CHUKI JUU YA WATOTO WA MME WAKE NA MARANYINGINE AKITENGENEZA SUMU, YA KUWAFUNDISHA WANAE( WATOTO WAKE MAMA WA KAMBO), JINSI YA KUWAKANDAMIZA NA KUWADHARAU WATOTO WA MMEWE.
HUO SIO UNGWANA KWA MWANAMKE MWENYE AKILI NA KUAMINI KWAMBA NA YEYE ANAWEZA KUACHA YATIMA, NA WAKAKABILIANA (WATOTO WAKE BAADA YA KIFO CHAKE) NA MATESO AMBAYO AMEWAPA WATOTO WA MKE MWENZA.


QURAN:
NABII MUHAMMAD (S.A.W)ALIKUWA YATIMA


MWNYEZI MUNGU ANASEMA

“NAAPA KWA MCHANA.
NA KWA USIKU UNAPOTANDA.
HAKUKUKUACHA MOLA WAKO WALA HAKUKASIRIKA
(NAWE EWE NABII MUHAMMAD).
NA BILA SHAKA (KILA) WAKATIA UJAO (UTAKUWA) NI BORA KWAKO KULIKO ULIOTANGULIA.
NA MOLA WAKO ATAKUPA MPAKA URIDHIKE.
JE! HAKUKUKUTA YATIMA AKAKUPA MAKAZI (MAZURI YA KUKAA)?
NA AKAKUKUTA FAKIRI AKAKUTAJIRISHA?
BASI USIMUONEE YATIMA.
WALA USIMKARIPIE AULIZAYE.
NA NEEME YA MOLA WAKO ISIMULIE (KWA KUMSHUKURU NA KWA KUFANYA AMALI NJEMA)”.

(SURATUDH DHUHAA)



NDIO MAANA ASILIMIA KUBWA DUNIANI YA WATOTO WA MTAANI, IMETOKANA NA VIFO VYA UPANDE WA WAKINA MAMA. NA ASILIMIA KUBWA DUNIANI YA WATOTO WA VITUONI NA MARABARANI, NA WENGINE KAMA MAKAHABA, MAISHA MABAYA NA MAGUMU YA WATOTO WA KIKE DUNIANI, ASILIMIA KUBWA YA MAMBO HAYO YAMETENGENEZWA NA KIWANDA CHA MAMA WA KAMBO KATIKA MSINGI WA UPUNGUFU AU UKOSEFU WA HURUMA MAJUMBANI MWAO.

HATUMAANISHI KWAMBA HAKUNA MAMA WA KAMBO WENYE MSINGI WA MALEZI BORA NA UKUTA WA HURUMA NA NGUZO YA ELIMU !! LA !! BALI NI WACHACHE NA WAWE NI WACHA MUNGU WA KWELI. MWANAMKE MCHA MUNGU HUWA NA MOYO WA HURUMA NA MSINGI WA MAISHA YAKE NI UVUMILIVU. MWANAMKE MCHA MUNGU HUWA NI MWENYE KUVUMILIA KATIKA MSINGI WA MANENO NA MATENDO NA HUWA MWEPESI KUSAMEHE NA KUOMBA MSAMAHA BILA KUJALI UMRI AU CHEO.

UTULIVU WA MAPENZI WA MAMA WA KAMBO NDIO MSINGI WA UTULIVU NA AMANI JUU YA MTOTO AU WATOTO YATIMA NDANI YA NYUMBA HUSIKA.


***MCHANGO WA UKOO KATIKA MALEZI YA WATOTO AMBAO WAMEACHWA NA NDUGU ZAO, KATIKA MAZINGIRA YA UYATIMA.************************** NI NINI ?

LAZIMA KWANZA TUJUWE NI NINI MAANA YA UKOO ?
UKOO NI MUUNGANO WA NAFSI NYINGI ZENYE UHUSIANO WA DAMU. BABA NA MAMA NDIO MSINGI WA KUANZISHA UKOO BORA AU UKOO MBAYA. KWA UPANDE MWINGINE UKOO NI MUUNGANO WA FAMILIA NYINGI. KUNA WATALAMU WENYE KUJUWA MAMBO HAYO YA KOO, SISI SIO WATALAMU WA NASABA.

SIKUZOTE, KILA BINADAMU ANAPENDA KUISHI KATIKA MAZINGIRA MAZURI NA KUISHI KATIKA JENGO LA AMANI NA UTULIVU MAISHANI MWAKE.

NI VYEMA NA NI MUHIMU, JUU YA KILA MZAZI KUAMINI KWAMBA YEYE NI MSINGI WA ULINZI NA UKUTA WA AMANI NA NGUZO YA UTULIVU JUU YA FAMILIA YAKE.

MALEZI NA MAELEKEZO BORA YA WAZAZI YANATOA FURSA YA UPENDO BAINA YA NDUGU, JAMAA NA MARAFIKI, KUWAPENDA WATOTO HUSIKA NA WATOTO KUWAPENDA NDUGU,JAMAA NA MARAFIKI.

UBOVU WA FAMILIA UNATOKANA NA NGUZO ZA FAMILIA. NGUZO ZA FAMILIA NI MME NA MKE. IKWA MWANAUME AMEMUOA MWANAMKE KWA KUTUMIA VIGEZO VYA KIMAHABA, BASI MKEWE ATAMUENDESHA KATIKA NJIA YA KIMAHABA. NA IKIWA MWANAUME ALIMUOA MWANAMKE KWA LENGO LA UBORA WA TABIA NJEMA KATIKA MATENDO NA MAONGEZI, BASI FAMILIA YAO ITAKUWA HODARI KATIKA KUONGEA NA KUKAMILISHA MAONGEZI KATIKA MSINGI WA MATENDO BORA.

KUMBUKA SIFA YA FAMILIA INATOKANA NA MATENDO NA MANENO YAKE, KATIKA JAMII.
NA KUMBUKA KWAMBA FAMILIA NDIO ALAMA YA KUONESHA HESHIMA YA KOO ZAKE. IKIWA MWANAMKE NI MBOVU TAYARI ANALETA DOA JUU YA FAMILIA YAKE NA UKOO WAKE, NA KWA UPANDE WA MWANAUME NDIVYO ILIVYO. FAMILIA BORA NI ILE YENYE KUSIFIWA NA KILA JIRANI YAKE NA KUPAMBWA AU KUSIFIWA NA WAGENI WANAOTEMBELEA NYUMBA HUSIKA.


IKIWA MSINGI WA UKOO HUSIKA, UNA BARABARA NJEMA YA AMANI, UPENDO, UTULIVU NA ELIMU YA KUTOSHA KUHUSU MAZINGIRA YA DUNIA, NIRAHISI SANA, KULINDA NA KUTETEA HAKI ZA WATOTO WAO WA YATIMA.

WATOTO YATIMA WANAWEZA KUSALIMIKA, NA KUISHI KATIKA MAZINGIRA MAZURI, PALE AMBAPO, KOO ZAO(UKOO WA UPANDE WA BABA NA UPANDE WA MAMA) ZINASHIRIKIANA KATIKA MSINGI WA UPENDO. KUMBUKA YA KWAMBA UPENDO HAUPATIKANI PASINA HURUMA. NA KUMBUKA HURUMA MSINGI WAKE NI UVUMILIVU NA UVUMILIVU UKUTA WAKE NI AMANI NA UWANJA WA AMANI NI UTULIVU.

UTULIVU UNAPOKUWEPO KATIKA KOO, LAZIMA KILA NAFSI ITAKUWA YA KWANZA KUSONONEKA, KWANZA KWA KUMPOTEZA NDUGU MPENDWA NA PILI KWA KUHURUMIA WATOTO AU MTOTO ALIYEBAKI KATIKA MAZINGIRA YENYE KUHITAJI MUONGOZO WA MAMA AU BABA MAISHANI.

UKOO WENYE UPENDO UTAFANYA KIKAO, NA KUCHUKUWA MAAMUZI YENYE MAZINGIRA MAZURI YA KUHAKIKISHA KWAMBA HUYO MTOTO YATIMA, ATAISHI KATIKA MAZINGIRA YA UPENDO, ULINZI, AMANI NA KUPATA HAKI YA ELIMU NA HAKI YA KUTOA MAONI NA KUPEWA MAJIBU YENYE MSINGI WA UFAHAMU BORA KATIKA UKOO AU KOO HUSIKA(YANI MTOTO WA YATIMA KUPEWA FURSA YA KUPANZA SAUTI KATIKA KOO ZOTE MBILI).

JE ! KOO ZOTE MBILI ZINAWAJIBIKA AU ZINAWEZA KUWAJIBIKA KATIKA MALEZI BORA YA YATIMA ?

NI NINI MAANA YA KOO ZOTE MBILI ?

MFUMO WA NDOA, MARANYINGI UNATOKANA NA KOO MBILI TOFAUTI. UTAMKUTA MAMA ANA UKOO WAKE NA BABA ANA UKOO WAKE. KUMBUKA YA KWAMBA KIUNGANISHI CHA KOO NI NDOA NA MUHURI (ALAMA) WA MUUNGANO WA KOO HUSIKA NI KIZAZI
(MTOTO AU WATOTO).

IKIWA KOO HUSIKA KATIKA MUUNGANO WENYE MSINGI WA NDOA, ZITAKUWA NA UPENDO, ULINZI, MALEZI BORA NA HURUMA JUU YA WATOTO WAO, AMBAO NI MUOAJI(MWANAMUME) NA MUOLEWA(MWANAMKE), BASI KITAKACHOFUATA, KOO ZOTE MBILI ZITASHIRIKIANA KATIKA KILA HALI, BILA KUJALI FURAHA, MAUMIVU, PESA, MALI,……….N.K, NA KUHAKIKISHA USALAMA WENYE MAZINGIRA YA UPENDO, AMANI NA UTULIVU, UNADUMU KATIKA MUUNGANO HUSIKA.

NA NDIOMAANA KILA UKOO UNAKUWA NA WATU WAZIMA NA WENYE AKILI TIMAMU, WENYE KUSIMAMIA, KUUNGANISHA, KUONDOA TOFAUTI ZA CHUKI NA KULINDA HAKI YA KILA UKOO NA KUSIMAMIA BENDERA
(KIUNGANISHI NI NDOA NA BENDERA KUU NI MTOTO AU WATOTO) YA MUUNGANO WA KOO ZOTE HUSIKA.

MWANAUME ANAPOFUNGA NDOA, NDUGU, JAMAA, NA MARAFIKI WANASHEHEREKEA MUUNGANO(NDOA) HUSIKA. LAKINI KINACHO BAKI NI SIRI YA KUWA KIZAZI KIPO?

MWANAMKE MWENYE KUOLEWA NA KUPATA MTOTO, HUWA NA UMUHIMU NA NGUVU KATIKA KOO ZOTE HUSIKA. NA MWANAMKE MWENYE UKOSEFU WA BENDERA(MTOTO), HUWA NI MWENYE KUJIHISI VIBAYA NA MARANYINGINE AKISIMANGWA NA WANACHAMA WA UKOO WA UPANDE WA MMEWE, NA MARANYINGINE HUJIKUTA AKIKUMBANA NA MAADUI KUTOKA UPANDE WA UKOO WAKE, WAKIMUONA YA KWAMBA NI TASA WALA HANA UWEZO WA KUPATA MTOTO. LAKINI KUMBUKA YA KWAMBA KUMPATA MTOTO NA KUMKOSA(KUKOSA KIZAZI) YOTE HAYO YANATOKANA NA UWEZA WA MWENYEZI MUNGU. KUNA BAADHI YA WANAWAKE WANAOKOSA KIZAZI, KUTOKANA NA NJIA YAO YA UTOWAJI WA MIMBA. MARANYINGI UTOAJI WA MIMBA UNAHARIBU KIZAZI.

IKIWA KOO ZOTE MBILI ZITAKUWA NA MAZINGIRA MAZURI YA KUONEANA HURUMA NA MSINGI WA KULINDA HESHIMA YAKE KATIKA JAMII, BASI HAKUNA UKOO AMBAO UTAKUBALI AU KURUHUSU WATOTO WAKE WA YATIMA, KUHANGAIKA KATIKA VITUO VYA YATIMA AU KUZURURA BARABARANI(WATOTO WA MTAANI) OVYO OVYO BARABARANI BILA KUWA NA DIRA YENYE MFUMO WA MALEZI NA MSINGI WA MAISHA BORA NA UKUTA WA ELIMU BORA KWA KILA MWANA CHAMA WA KOO HUSIKA.

UPUNGUFU WA UPENDO KATIKA KOO, NDICHO CHANZO CHA MGAWANYIKO WA MAPENZI KATIKA NYOYO ZA WANACHAMA WA KOO HUSIKA.

MATUNDA YA UKOO BAADA YA MSAADA WA MALEZI JUU YA MTOTO AU WATOTO YA TIMA****NI NINI ?

KILA MTU ANAPENDA KUTOA SHUKURANI PALE ALIPOSAIDIWA NA KULAUMU PALE ALIPOUMIZWA. KWA MUJIBU WA MAISHANI, KILA JAMBO MAISHANI MWETU LINAHITAJI ELIMU YA KUTOSHA ILI KUKABILIANA NALO, BILA KUSABABISHA BADHARA YENYE JINA LA SIKUJUWA A.K NAJUTA KULIFANYA.

UKIWASAIDIA WATOTO AU MTOTO WA YATIMA. TAYARI UNAPATA THAWABU, NA UMETOA MCHANGO WA KUPUNGUZA WEZI, MAKAHABA, WAKABAJI, WABAKAJI, MATAPELI, WATOTO WA MTAANI, MARADHI KAMA UKIMWI, TIBI, HASIRA, CHUKI, LAWAMA, FITINA………N.K. YOTE HAYO UTAKUWA UMEAYASAIDIA KATIKA JAMII. KILA JAMBO AMBALO MWENYEZI MUNGU ANATUKATAZA LINAMAFUFA JUU YETU BINADAMU WOTE, NA LILE TUNALOKATAZWA NINA MADHARA JUU YETU SOTE.

MTOTO YATIMA ANAPOKOSA MSAADA NA AKADHULUMIWA NA WANACHAMA WA KOO ZOTE (UPANDE WA BABA NA MAMA), MARANYINGI ANABADILIKA KIAKILI NA KIVITENDO. IKIWA NI MTOTO WA KIKE, ATAAMUA KUTUMIA MWILI WAKE ANAVYO JUWA, ILIMRADI AKIDHI MAHITAJI YAKE, NA PALE ANAPOKUWA ANAISHI NA WADOGO ZAKE, JITIHADA ZITAKUWEPO ZA KUBADILI WANAUME NA KUFANYA KILA AINA YA KAZI ILIMRADI APATE KIPATO CHA KUWALISHA WADOGO ZAKE NA KUWASOMESHA. MATOKEO YAKE HUJIKUTA AKIKUMBANA NA MIMBA ZENYE MSINGI WA SIMJUI BABA YAKO, TAYARI AMEISHA TENGENEZA VITA NYINGINE BAINA YAKE NA MTOTO WA HARAMU. AKIJIZUIA AKITUMIA KINGA ATAJIKUTA AKIKOSA HESHIMA, NA AKIMUACHA MUNGU WAKE KATIKA MASAFA MAREFU. AKISEMA ASIFANYE UKAHABA HAKUNA MTU YEYOTE KATIKA JAMII MWENYE KUMSAIDIA KATIKA KATIKA MAZINGIRA HAYO MAGUMU. NA AKIANGALIA PEMBENI KANISANI AU MSIKITINI HAKUNA MFUKO WA MATIBABU, MAVAZI, KUWASOMESHA AU KUWALISHA WATOTO WA YATIMA. AKIGEUKA AMEKUMBANA NA MISTA UKIMWI KWENYE KONA. AKITAFAKARI, BINAADAMU KAMA KAWAIDA YAO, MUONE AMEATHIRIKA, KWANZA ALIKUWA AKILINGA…..AKIINAMA KWA MAUMIVU ANAKUMBANA NA RIPOTI YA CHAKU, ADA, KODI YA NYUMBA……N.K. HAYA NDIO MAISHA YA WATOTO YATIMA. HAYANA MWISHO KATIKA MAELEZO, KWASABABU KILA MTOTO WA YATIMA ANAUPEO WA KUJUWA MAPENZI YA WATU ZAIDI YA WATU WANAVYO JIJUWA.


WATOTO YATIMA NI RAHISI SANA KUKUMBUKA FADHILA JUU YAWALE WALIOWAPA AU KUWAONESHA NJIA YA WEMA NA NIRAHISI KUONDOA UPENDO JUU YA KILA MTU WANAOMFAHAMU KATIFA KOO ZAO, AMBAYE HAJAWASAIDI HATA KIKOMBE CHA MAJI AU MAWAZI YENYE MSINGI WA FARAJA. NDIO MAANA MWENYEZI MUNGU ANATUHIMIZA KUWA NA SUBIRA(UVUMILIVU) MAISHANI MWETU. BILA SUBIRA DUNIA HII INGEWAKA MOTO KWA KULIPIZA KISASI, NAFIKIRI HOSPITALI, MAGEREZA, VITUO VYA POLISI NA MAKABURINI KUNGEKUWA BIZE. LAKINI KUTOKANA NA NGUVU ZA MWENYEZI MUNGU, AMECHANGANYA WATU WENYE WIVU, CHUKI, LAWAMA, HUSUDA PAMOJA NA WANAWAKE NA WANAUME, WENYE MOYO WAKUWAONEA WATOTO YATIMA HURUMA NA KUWASAIDIA MAHITAJI YAO. UNAPOMSAIDIA MTOTO WA YATIMA MAISHANI MWAKE, TAYARI UMEMTANDIKIA LAMI KATIKA NJIA YAKE. NJIA PANDA YENYE LAMI HUWA NI BORA KULIKO NJIA PANDA YENYE MABONE YA CHUKI, FITINA, WIVU, LAWAMA, HASIRA, UADUI…………N.K.

MTUME MUHAMMAD(S.A.W) ALISEMA

“NYUMBA MBAYA YA KIISLAMU NI ILE AMBAYO INAMTESA MTOTO WA YATIMA. NA NYUMBA NZURI YA KIISLAMU NI ILE AMBAYO INAMLEA MTOTO YATIMA KATIKA MAZINGIRA MAZURI”




MTUME MUHAMMAD(S.A.W) ALISEMA


“UKIMLEA MTOTO WA YATIMA VIZURI UTAKUWA SAMBAMBA NA MTUME MUHAMMAD (S.A.W) PEPONI”

Thursday, August 27, 2009

BISMILLAHIR RAHMANIR RAHIM 22/08/09




UTANGULIZI:
SIFA ZOTE NJEMA ANASTAHIKI MWENYEZI MUNGU MOLA WA VIUMBE VYOTE. NA REHMA NA AMANI ZIMSHUKIE MTUME WETU MUHAMMAD (S.A.W) NA JAMAA ZAKE NA MASWAHABA WAKE WOTE. NYARAKA HIZI ZIMEKUSANYA HUKUMU ZILIZOKUWA LAZIMA KUZIJUA KWA KILA MFUNGAJI WA MWEZI WA RAMADHANI, ILI MFUNGAJI AWE NA UJUZI KAMILI KATIKA KUTEKELEZA IBADA HII TUKUFU YA SWAUMU YA MWEZI WA RAMADHANI. KWAHIVYO NDUGU MUISLAMU, JITAHIDI SANA KUZISOMA NYARAKA HIZI KWA MAKINI SANA NA UYAELEWE YALIYOMO. NAOMBA MWENYEZI MUNGU ATUFANYIE WEPESI KATIKA KUZIJUA HUKUMU ZA KUFUNGA.

1) HUKUMU YA KUFUNGA
KUFUNGA KATIKA MWEZI WA RAMADHANI NI FARADHI (LAZIMA) KWA KILA MUISLAM ALIYEBALEHE, MWENYE AKILI TIMAMU NA MWENYE KUWAJIBIKA KUFUNGA.


2) MAANA YA KUFUNGA KATIKA SHARIA YA KIISLAM.
MAANA YA KUFUNGA KATIKA SHARIA YA KIISLAMU NI KUJIZUIA NA YOTE YANAYOFUNGUZA, KUANZIA ALFAJIRI YA KWELI, MPAKA MAGHARIBI, PAMOJA NA KUTIA NIA YA KUFUNGA USIKU.

3) NGUZO ZA KUFUNGA (SWAUMU) NI MBILI (2)

NGUZO ZA KUFUNGA NI MBILI:
NGUZO YA KWANZA NI :
1) KUTIA NIA YA KUFUNGA USIKU KATIKA SIKU ZOTE ZA MWEZI WA RAMADHANI. NIA NI DHAMIRA ANAYOKUA NAYO MTU MOYONI MWAKE KUWA ATAFUNGA, NIA MAHALA PAKE NI MOYONI.
MFUNGAJI ANALAZIMIKA KUTIA NA YA KUFUNGA KILASIKU USIKU KATIKA MWEZI WOTE WA RAMADHANI. MWANZO WA NIA NI BAADA YA KUFUTURU HADI MWISHO WA KULA YAANI MWISHO WA KULADAKU, NDIO MWISHO WA KUTIA NIA. KWA HIVYO MWENYE KUFUNGA BILA YA KUTIA NIA (KUNUWIYA) FUNGA YAKE NI BATILI.





NGUZO YA PILI NI :
2) KUJIZUIA NA YOTE YANAYOFUNGUZA KUANZIA ALFAJIRI YA KWELI MPAKA MAGHARIBI.

4) MASHARTI YA KUWAJIBIKA KUFUNGA

MASHARTI YA KUWAJIBIKA KUFUNGA NI KAMA IFUATAVYO :

1) MFUNGAJI AWE MUISLAM.
2) AWE NA AKILI TIMAMU
3) AWE NA UWEZO WA KUFUNGA KIAFYA.(ASIWE MGONJWA).
4) AWE MKAZI WA MJI (ASIWE MSAFIRI).
5) AWE AMEBALEHE.
6) ASIWE KATIKA HEDHI AU NIFASI.


5) MAMBO YANAYOHARIBU SWAUMU (YANAFUNGUZA)
MFUNGAJI LAZIMA AJIZUIE NA VITENDO VINAVYOWEZA KUHARIBU SWAUMU (FUNGA) YAKE.
MAMBO YANAYOHARIBU SWAUMU NI HAYA HAPA YAFUATAYO:
1) KULA AU KUNYWA KWA MAKUSUDI.
2) KUJITAPISHA KWA MAKUSUDI.
3) KUJITOA MANII(MBEGU ZA UZAZI) KWA MAKUSUDI.
4) KUFANYA TENDO LA NDOA(KUJAMIIANA) MCHANA WA RAMADHANI.
5) KUINGIZA KITU CHOCHOTE KATIKA TUNDU SABA ZA MWILI KWA MAKUSUDI(MAKUSUDIO YA TUNDU SABA ZA MWILI, NI TUNDU MBILI ZA MASIKIO, TUNDU MBILI ZA PUA , MDOMO, SEHEMU INAPOTOKA HAJA KUBWA NA SEHEMU INAPOTOKA HAJA NDOGO).
6) KUNUWIA KUFUNGULIA. MFUNGAJI AKINUWIA KUFUNGULIA HATA KAMA HAKUFUNGULIA SWAUMU YAKE ITAHARIBIKA.
7) KUVUTA SIGARA.
8) KUBWIA UGORO
9) KUNUSA TUMBAKU
10) KUPATWA NA WAZIMU
11) KUTAFUNA TAMBUU
12) KURTADDI (KUTOKA KATIKA UISLAMU)
13) KUPATWA NA HEDHI
14) KUPATWA NA NIFASI.


PAMOJA NA HAYA PIA, MFUNGAJI NI LAZIMA AJIEPUSHE MAASI YOTE KAMA VILE :
KUACHA SWALA, ULEVI, WIZI, DHULMA, RUSHWA, UTAPELI, UONGO,UMBEYA, KUSENGENYA, KUTUKANA, KUGOMBANA, KUPIGA POROJO, KUSIKILIZA ALIYOYAKATAZA MWENYEZI MUNGU. KWA UFUPI NI KWAMBA , MFUNGAJ ANTAKIWA AJIEPUSHE NA KILA KITENDO KITAKACHOPELEKEA KUVUNJA AMRI YA MWENYEZI MUNGU NA MTUME WA MUHAMMAD (S.A.W). KWANI KUFUNGA SI KUACHA KULA NA KUNYWA TU BALI KUFUNGA NI KUACHA KULA NA KUNYWA NA MAASI YOTE NILIYOYATAJA, KINYUME CHA HAYO HAKUNA FUNGA, BALI NI KUSHINDA NA NJAA PAMOJA NA KIU.
KWA HIYO EWE MFUNGAJI KUWA MAKINI JUU YA HAYA, USIJE UKAIHARIBU FUNGA YAKO KWA KUTENDA MAASI HAYA NILIYOYATAJA.

6) MAMBO YASIYOHARIBU SWAUMU(FUNGA)

HAITAHARIBIKA SWAUMU KWA MATENDO YA FUATAYO:
1) KULA AU KUNYWA KWA KUSAHAU AU KWA KULAZIMISHWA KIASI CHA KUTISHIA MAISHA.
2) KUTAPIKA BILA KUKUSUDIA
3) KUTOKWA NA MANII(MBEGU ZA UZAZI) KWA KUOTA AU KWA NAMNA AMBAYO HAKUKUSUDIA.
4) KUOGA MCHANA WA RAMADHANI AU WAKATI WOWOTE.
5) KUAMKA NA JANABA
6) KUPIGA MSWAKI
7) KUSUKUTUA
8) KUTIA DAWA YA MACHO
9) KUPAKA WANJA
10) KUUMIKA (KUPIGA CHUKU)
11) KUJIPAKA MAFUTA AU MANUKATO
12) KUPIGA SINDANO
13) KUWEKA DAWA KWENYE JERAHA.
14) KUTOKA DAMU AU USAHA KWENYE JERAHA AU KWA KUJIKATA
15) KUTUMBUA JIPU
16) KUCHEKA
17) KULALA
18) KUNG’OA JINO
19) KULIA

7) WANAORUHUSIWA KULA MCHANA WA RAMADHANI KWA MUJIBU WA SHARIA YA KIISLAM NI HAWA WAFUATAO :

1) MGONJWA : MTU AKIJIONA MGONJWA HANA AFYA NZURI YA KUMUWEZESHA KUFUNGA, ANARUHUSIWA KULA, KISHA ATALIPA AKIPONA UGONJWA WAKE. NA KAMA UGONJWA WAKE NI WA KUDUMU USIOTARAJIWA KUPONA, ATATOA FIDIA AMBAYO NI KIBABA KIMOJA CHA CHAKULA KUWAPA MASIKINI KILA SIKU KATIKA MWEZI WOTE WA RAMADHANI.
KIBABA KIMOJA NI SAWA NA KAMA KILO KASROBO YA CHAKULA KINACHOTUMIWA SANA, KATIKA MJI HUSIKA KAMA HAPA KWETU (DAR ES SALAAM NA PWANI) NI MCHELE.

2) MSAFIRI : MTU AKIWA SAFARINI ANARUHUSIWA KULA KISHA ATALIPA SIKU ALIZOKULA AKIWA SAFARINI. SAFARI AMBAYO MTU ANARUHUSIWA ASIFUNGE NI SAFARI INAYOANZIA UMBALI WA KILOMITA THAMANINI NA MOJA (81 KMS)
3) MZEE : MTU MZIMA (KIKONGWE AU AJUZA) AMBAE HAWEZI KUFUNGA KWA SABABU YA UZEE, ANARUHUSIWA KULA, NA BADALA YAKE ATATOA FIDIA AMBAYO NI KIBABA CHA CHAKULA, KUMPA MASIKINI KILA SIKU, KATIKA MWEZI WOTE WA RAMADHANI.
4) MJAMZITO NA MWENYE KUNYONYESHA
MWANAMKE MJAMZITO AU ANAYENYONYESHA WANARUHUSIWA KULA, KISHA WATALIPA SIKU WALIZOKULA BAADA YA KUJIFUNGUWA NA KUACHISHA ZIWA.

8) MWANAMKE MWENYE HEDHI AU NIFASI
MWANAMKE ALIYE KATIKA HEDHI AU NIFASI NI HARAMU KWAKE KUFUNGA MPAKA ATAKAPOTAKASIKA NA ATALAZIMIKA KULIPA SIKU ALIZOACHA BAADA YA KUKATIKA HEDHI YAKE AU NIFASI YAKE.
9) SUNNA ZINAZOAMBATANA NA FUNGA YA RAMADHANI
KATIKA MWEZI WA RAMADHANI KUNA MAMBO KADHAA ALIYOYAFANYA MTUME (S.A.W) NA KUTUSISITIZA NASI TUYAFANYE. MIONGONI MWA MAMBO HAYO NI KAMA IFUATAVYO:
1) KULA DAKU NA KUCHELEWESHA
DAKU NI CHAKULA KINACHOLIWA USIKU WA MANANE KWA AJILI YA KUJIANDAA KUFUNGA SIKU INAYOFUATA. KULA DAKU NI SUNNA ILIYOKOKOTOZWA NA MTUME (S.A.W). VILEVILE NI SUNNA KUCHELEWESHA KULA DAKU. KILA INAPOLIWA DAKU KARIBU ZAIDI NA ALFAJIRI NDIVYO INAVYOKUA BORA ZAIDI.
2) KUHARAKISHA KUFUTURU(KUFUTURU MAPEMA)
NI “SUNNA ILIYOKOKOTEZWA” KUFANYA HARAKA KUFUTURU MARA LINAPOKUCHWA JUA NA KABLA YA SWALA YA MAGHARIBI. PIA NI SUNNA KUANZA KUFUTURU KWA TENDE AU KWA MAJI.
3) KUOMBA DUA WAKATI WA KUFUTURU.
NI SUNNA KUOMBA DUA WAKATI WA KUFUTURU KAMA VILE KUOMBA KWA KUSEMA : « EWE MOLA WANGU NIMEFUNGA KWA AJILI YAKO NA NIMEFUNGULIA RIZIKI YAKO «
4) KUSOMA QUR-AN
5) KUTOA SADAKA KWA WINGI
6) KUSWALI SWALA YA TARAWEHE
7) KUZIDISHA KUTENDA MAMBO YA KHERI. KAMA VILE KUMFUTURISHA ALIYEFUNGA, KUSAIDIA MAYATIMA, KUSAIDIA WENYE MATATIZO,N.K.
8) KUZIDISHA KUFANYA IBADA KATIKA KUMI LA MWISHO
9) KUKAA ITIKAFU KATIKA KUMI LA MWISHO
10) KUUTAFUTA USIKU MTUKUFU WA LAILATUL QADRI KATIKA KUMI LA MWISHO.


HITIMISHO :
NIMEGUNDUA KWAMBA BAADHI YA WAUMINI WANAOFUNGA MWEZI WA RAMADHANI, KWAMBA HAWASWALI SWALA TANO. KUACHA KUSWALI NI KOSA KUBWA LINALOWEZA KUMTOA MTU KATIKA DINI YA KIISLAM. KWA HIVYO, WALE WENYETABIA YA KUFUNGA TU BILA KUSWALI WAACHE TABIA HIYO, BALI WAFUNGE PAMOJA NA KUSWALI SWALA TANO SIKU ZOTE, NA SIO KUSWALI KATIKA MWEZI WA RAMADHANI TU.


WABILLAH TAUFIQ
IMEANDIKWA NA :
ALLY MUHIDINI MKOYOGORE
IMAM WA MASJID SWAHILINA
KINONDONI MOROCCO BLOCK 41
NA USTADH KATIKA MASJID
AL – QADIRIYYA TEMEKE
WAILES MTAA WA CHANGANI
P.O.BOX : 45635
KWA MAONI, MASWALI TUMIA NJIA YA SIMU YA MKONONI AU POSTA.
MOB : 0787 73 04 30
OR
0767 73 04 30

From Babati with a goat


From Babati with a goat: Our photographer Ramadhani Chitanda captured Agnes at Sanawari just before she boarded a bus to Moshi with a goat stuffed in her basket. The goat is a gift from her mother who resides in Babati to Agnes's sister married in Moshi.


A petty storm caused by an afternoon downpour recently was enough to wash away part of the brick wall and iron bars fence recently erected around the Azimio la Arusha Museum in Kaloleni area by a Dar es Salaam contractor. (Photo by Ramadhani Chitanda)
Strong winds last week blew off the roof of two classrooms at Njiro Hill Primary School. But as a stop gap measure of more of such incidents, ANEPO donated 150 tree seedlings to be planted in the school's compound by school children and their teachers. (Photo by Raymond John)


A resident of Ilboru, Raheri Simon, was seriously injured when she was knocked down by a car along Makongoro Road on March 23. She was hit by a Toyota Mark II with registration numbers T656 ADG.
Sister Mary Rashmi officially opening Zinduka Women Group celebrations on March 18 in Njiro. The event was part of the Women's day commemoration marked worldwide on March 8. The organization brings together 21 small groups from Arusha region engaged in economic activities. (Photo by Ramadhani Chitanda)


Grinding Poverty: Nasikaki Mollel of Bangata in Arumeru has just finished selling a head-load of bananas but what she has earned for the day is peanuts compared to her daily obligations at home. She has earned hardly Tsh.1,000 and if she boards a bus to Ngulelo she will have a balance of only Tsh.800

The Month of Mercy and Forgiveness


Praise be to Allah, the Lord of the Worlds; and blessings and peace be upon our Prophet Muhammad and upon all his Family and Companions.
Allah, the Alone, Creator of all times and all places, gives priority to some places over some other places and some periods over some other periods.

Once again the blessed month of Rajab is upon us. It opens the series of three holy months culminating in Ramadhan: Rajab, Shaban, and Ramadhan. During these three months everyone must prepare themselves and keep themselves as much as possible away from bad manners and sins.

Our beloved prophet said "Rajab is the month of Allah, Shaban is my month and Ramadhan is the month of my community." Allah gave us twelve months in the year, eleven of which are ours and one of which belongs to him. What rewards Allah will give his servants in His month no one knows, not even the prophets. The work of prophets and angels stops in the month of Rajab. They are not allowed to know what reward Allah is going to give to his community. In the following month, shaban, no one is permitted to know what rewards the prophet Muhammad (peace and blessing be upon him) will give his community except himself and Allah.

Allah Says (interpretation of meaning): {And your Lord creates whatsoever He wills and chooses, no choice have they (in any matter). Glorified be Allâh, and exalted above all that they associate as partners (with Him).}[28: 68>. Allah gives preference of some nights over other nights and of some days over other days. Lailat al-Qadar (Night Of Power) is among the virtuous nights and it is the most virtuous of all nights. Allah Says about this night (interpretation of meaning): {The night of Al-Qadr (Night Of Power) is better than a thousand months (i.e. worshipping Allâh in that night is better than worshipping Him a thousand months, i.e. 83 years and 4 months).}[97: 3>.

The act of a person in this night is better than a thousand months. This night exists in the last ten days of the month of Ramadan. The Prophet (PBUH) said: "Search for it in the last ten days of the month of the Ramadan". [Bukhari and Muslim>.

The nights of the month of the Ramadan are among the virtuous nights in general and the nights of the last ten days in particular since the reward of the acts is multiplied in this month. The Prophet used to lighten his waist belt (i.e. work hard) and used to pray all the night, and used to keep his family awake for the prayers.


In general all the nights of a Muslim are excellent nights since Allah descends every night in the last third of the night and Says: Is there anyone to invoke Me that I may respond to his invocation? Is there anyone to ask Me so that I may grant him his request? Is there anyone asking My forgiveness, so that I may forgive him?"

The mentioned days and all the times of a Muslim are good and appropriate for worshipping Allah. But Allah gives preference to some times over some others only to make them an opportunity for doing good acts as much as possible and these acts are useful for the Muslim in this life and in the Hereafter life.
Celebrating the mentioned days means using them for doing good deeds as much as possible. One should use them for fasting, praying, supplicating Allah, avoiding all kinds of innovations practiced by many people who spend these times in amusement and other useless activities.
with our best wishes...

Nigeria kuwakamata zaidi vigogo wa benki


Kikosi maalum cha polisi wa kuzuia ubadhirifu nchini Nigeria kimesema kinajiandaa kawakamata zaidi wafanyabiashara wakubwa walioshindwa kulipa madeni ya mabilioni ya fedha wanayodaiwa katika benki mbalimbali.

Hatua hiyo inafuatia kumalizika kwa muda maalum uliokuwa umewekwa kuhakikisha wale wanaodaiwa wawe wamekwisharudisha fedha hizo kwa benki hizo zinazoelekea kufilisika.

Serikali ililazimika kuokoa benki tano na kuwafukuza kazi viongozi wote wa benki hizo wiki iliyopita katika juhudi za kuzuia benki hizo kuanguka.

Baadhi ya maafisa wa ngazi ya juu kabisa wa benki hizo wanashikiliwa na polisi, lakini wawili wangali mafichoni.

Maafisa hao wawili wanatafutwa na polisi kuhusiana na tuhuma za wizi wa pesa na ukiukwaji wa maadili ya utoaji mikopo.

Katika hali isiyokuwa ya kawaida, kikosi hicho maalum cha polisi pia kinawasaka wadaiwa.

Wiki iliyopita gavana wa benki kuu ya Nigeria aliwaaibisha hadharani baadhi ya matajiri wakubwa barani Afrika akiwataja kwa majina kwa kushindwa kulipa mikopo mikubwa waliokopa kutoka katika benki mabalimbali.

Maafisa wa kuzuia ubadhrifu wanasema baadhi ya fedha hizo zimerejeshwa, lakini kiasi kikubwa bado hakijarejeshwa.

Tarehe ya mwisho kurejesha fedha hizo ilipangwa kuwa Jumanne wiki hii.

Wengi wa wataalamu wa sheria wanasema kuwa deni ni suala ya kesi ya madai na hivyo wamekosoa kisheria uhalali wa kuwakamata wadaiwa.

Lakini mkuu wa kikosi cha polisi cha kuzuia ubadhrifu, Farida Waziri anasisitiza kuwa kuna kesi ya kujibu.

''Tunaweza kuwakamata maafisa hao kwa kula njama pamoja na wafanyakazi wa benki mbalimbali.''

''Baadhi ya mikopo ilitolewa pasipo utaratibu, na baadhi ilitolewa katika mazingira ya udanganyifu,'' amesema

Aliendelea kwa kuzitaka mahakama kutotoa kile alichokiita ,haki ya kuwalinda wadaiwa.

Amesema kuwa anatambua kuwa wadaiwa hao wapo mahali wakifanya mikutano ya siri na wamekuwa na mipango ya kuishitaki serikali.

Hawa ni kundi la watu wenye nguvu na nia moja walio tayari kupambana kulinda maslahi yao binafsi.

Lakini kikosi maalum cha kuzuia ubadhirifu cha Nigeria chenyewe kina utata.

Wanakosolewa kwa kiwango kikubwa nchini Nigeria kwa kupoteza mwelekeo katika vita dhidi ya rushwa kutokana na kusisitiza kwao kwamba, wadaiwa walipe madeni moja kwa moja kwa kikosi hicho kwa njia ya hundi za mamilioni ya dola za kimarekani.

Muswada haki za wanawake Mali watupwa


Rais wa Mali ametangaza hatatia saini muswada mpya wa sheria inayohusu familia na badala yake ataurejesha tena muswda huo bungeni ili uweze kupitiwa upya.

Makundi ya Kiislamu yamekuwa yakipinga sheria hiyo inayowapa haki kubwa wanawake tangu bunge lilipoupitisha mwanzoni mwa mwezi huu.

Rais Amadou Toumani Toure amesema anaurejesha muswada huo bungeni kwa manufaa ya umoja wa taifa.

Viongozi wa Kiislamu wameielezea sheria hiyo ni kazi ya shetani ni ni kinyume na Uislamu.

Zaidi ya asilimia 90 ya wananchi wa Mali ni Waislamu.

Baadhi ya vipengele ambavyo vimezua utata katika sheria hiyo vinawapa haki zaidi wanawake.

Matahalan chini ya sheria hiyo mpya, wanawake hawatakiwi kuwaheshimu waume wao na badala yake waume na wake wawe wanaheshimiana sawa.

Rais Amadou Toumani Toure amesema amechukua uamuzi huo kuhakikisha kunakuwa na utulivu na jamii yenye amani na halikadhalika aungwe mkono na raia wenzake.

Zimbabwe yakanusha Mugabe kuumwa


Maafisa nchini Zimbabwe wamekanusha taarifa kuwa rais Robert Mugabe ni mgonjwa, wakiziita taarifa hizo kuwa zenye nia ya uovu.

Gazeti la Times la Afrika Kusini limedai kuwa rais Mugabe alichukuliwa kwa siri na kupelekwa hospitali nchini Dubai kwa matibabu.

Lakini maafisa wa Zimbabwe wamesema kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 85, amerudi nchini Zimbabwe baada kuwa likizo nchini Dubai, akiwa na afya njema.

Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma anatarajiwa kuwasili nchini Zimbabwe siku ya Alhamis wiki hii kwa mazungumzo na rais Mugabe.

Msemaji wa Zuma amesema mkutano umepangwa kuendelea kama kawaida.

''Hatujapokea taarifa zozote rasmi kuhusu hali ya afya ya rais Mugabe, na kwa maana hiyo mipango yetu haijabadilika,'' amesema Vincent Magwenya.

UPUUZI MTUPU

Gazeti la Times liliripoti kuwa rais Mugabe amekuwa akifanyiwa matibabu maalum nchini Dubai.

Lakini maafisa wa Zimbabwe wamekanusha vikali madai hayo.

''Rais si mgonjwa, lakini alikuwa likizo,'' shirika la habari la Reuters lilimkariri afisa mmoja akisema.

''Amerudi nchini jana, na taarifa zote hizo ni upuuzi mtupu na mawazo dhaifu na ya uovu.''

Taarifa hizo zimekuja wakati rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma akijiandaa kufanya ziara yake ya kwanza akiwa kama rais nchini Zimbabwe.

Zuma ni mwenyekiti wa sasa wa nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADEC), chombo kilichosaidia kufanikisha kuundwa kwa serikali ya ushirikiano ya Zimbabwe.

Chama cha Bwana Tsvangirai cha Movement for Democratic Change (MDC) kimekuwa kikitoa malalmiko mbambali kuhusu utekelezaji wa mgawanyo wa madaraka ikijumuisha uteuzi wa rais Mugabe kwa gavana wa benki kuu na mwanasheria mkuu.

Chama hicho kimesema uteuzi huo umekiuka moja ya kanuni zinazotakiwa katika serikali hiyo ya umoja wa kitaifa.

Tuesday, August 25, 2009

Viongozi wakutana Addis Ababa


Hii itakuwa ni mara ya kwanza viongozi wa Afrika kukutana kwa ajili ya kuzungumzia maswala yanayohusiana na madadiliko ya hali ya anga, na kutaka kuyazungumzia kwa sauti moja.
Mkutano huu unaodhaminiwa na Umoja wa Afrika, unakusudiwa kusaidia nchi za Afrika kuwasilisha msimamo moja katika mkutano wa Umoja wa Mataifa wa kujadili mabadiliko ya hali ya anga utakaofanyika huko copenhangen, Denmark mwezi December mwaka huu.

Kufikia sasa, nchi mbalimbali barani Afrika zimewasilisha misimamo tofauti tofauti jambo ambalo wengi wanakusudia limechangia kutotiliwa maanani msimano wao.

Akizungumza na BBC, Daktari Alice Kaudia ambaye ni katibu katika wizara ya mazingira nchni Kenya alisema kwamba ilikuwa ni muhimu kwa nchi za Afrika kushirikiana katika jitihada za kukabiliana na mabadiliko ya hali ya anga.

Dk Kaudia alisisitiza kwamba matatizo yanayotokana na mabadiliko ya anga hayawezi kutatuliwa na nchi moja.

Mkutano huu unaoongozwa na mwenyekiti wa Umoja wa Afrika Muammar Gaddafi, unatarajiwa kujadili maswala mbali mbali yakiwemo pendekezo kwa nchi zilizoendelea kupunguza uchafuzi wa hewa kwa asilimia 40.

Kifo cha Michael Jackson ni dawa kali


Nyaraka za mahakama nchini Marekani zinaonyesha kuwa mwanamuziki Michael Jackson alikuwa akitibiwa ugonjwa wa kusikia mauvimu makali ya mwili na kutokupata usingizi.
Nyaraka za ofisi ya Mchunguzi wa Vifo vinavyotokea katika mazingira ya kutatanisha, zinaonyesha kuwa mwili wa mwanamuziki huyo ulikutwa na kiwango kikubwa cha dawa kali za kutuliza mauvmivu.

Ugunduzi huo unafuatia uchunguzi uliokuwa umefanyika kwa siri na ambao kwa sasa umewekwa bayana kwa jamii mjini Houston.

Mwanamuziki huyo alifariki tarehe 25 mwezi June mwaka huu akiwa na umri wa miaka 50, baada ya kupata mstuko wa moyo akiwa nyumbani kwake mjini Los Angeles.

Daktari wa Michael Jackson, Conrad Murray amekwisha hojiwa mara mbili na polisi lakini hajatamkwa rasmi kama ni mtuhumiwa.

Ofisi za Daktari Murray zilivamiwa na polisi mwezi uliopita ikiwa ni sehemu ya uchunguzi wa polisi juu ya kifo cha mwanamuziki huyo.

Wachunguzi wanajaribu kuangalia iwapo kuna kosa la kuua kwa kukusudia kutokana na uzembe kimatibabu, mwandishi wetu Rajesh Mirchandani aliyeko Los Angeles anasema.

Ofisi ya mchunguzi wa vifo vinavyotokea katika mazingira ya kutatanisha bado hajachapisha rasmi taarifa ya matokeo ya uchunguzi iliyopatikana juu kifo cha mwanamuziki huyo.

Na pia ofisi hiyo imeshindwa kuzungumza kuhusu taarifa kutoka shirika moja la habari kuwa chanzo kimoja kisichotajwa cha polisi kinasema kuwa mchunguzi wa vifo vinavvyotokana na mazingira ya kutatanisha amefikia uamuzi kuwa, kifo cha Michael Jackson ni cha kukusudiwa.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, ofisi ya Mchunguzi Mkuu wa vifo wa Los Angeles, ''amepitia kwa mara nyingine matokeo ya uchunguzi na taaarifa yake ya awali ni kwamba sababu ya kifo cha Michael Jackson ni matumizi ya kiwango kikubwa cha dawa za kutuliza mauvimu.''

Nyaraka hizo zinaendelea kusema kuwa Dr Murray aliwambia polisi kuwa amekuwa akimpa Michael Jackson dawa kali za kutuliza mauimvu ikiwa ni sehemu ya matibabu kwa ugonjwa wa kusikia mauvimu makali ya mwili na kutokupata usingizi.

Lakini alisema alikuwa na wasiwasi kuwa Michael Jackson alikuwa ameathirika kupenda kutumia dawa hizo kali na pia alikuwa akijitahidi kumzuia kwa kumshauri kutumia dawa mbadala.

Lakini asubuhi ya siku ya kifo cha mwanamuziki huyo, Dr Murray anaripotiwa kuwa alimpa Michael Jackson kiwango kidogo cha dawa hizo kali baada ya kuonekana kuwa dawa alizokuwa akitumia hazikufanya kazi.

Aliondoka na kumwacha mwanamuziki huyo peke yake kwa lengo la kupiga simu kadhaa, na ndipo aliporejea alikuta mwanamuziki huyo hawezi kupumua, gazeti la LA Times linataarifu.

Inafahamika kuwa Dr Murray alijaribu kumrudishia uwezo wa kupumua wakati wakisubiri gari la wagonjwa, lakini mwanamuziki huyo alitangazwa kuwa ameshakufa alipowasili hospitali.

Chupa za dawa kali za kutuliza maumivu zilizokutwa katika nyumba ya Michael Jackson zinaonyesha kuwa zilikuwa zimeidhinishwa na madaktari kadhaa, na si Conrad Murray peke yake, lakini bado anabakia kuwa mtu muhimu katika sula zima la uchunguzi, mwandishi wetu anaongeza.

Mapema mwezi huu, DR Murray aliyekuwa ameajiriwa kama Daktari binafsi wa mwanamuziki huyo kwa ajili ya matamasha kadhaa yaliyokuwa yafanyike jijini London mwezi Julai mwaka huu, ameweka mkanda wa video katika wavuti ya youtube kuwashukuru wanaomuunga mkono.

''Nimesema ukweli na nina imani kuwa ukweli utabakia kama ulivyo,'' alisema katika mkanda huo mfupi wa video wa dakika moja.

Monday, August 24, 2009

Kadhaa wauawa mapiganoni Somalia


Idadi kubwa ya watu wameuawa katika mapigano zaidi yaliyotokea Mogadishu mji mkuu wa Somalia, kati ya wanamgambo wa al Shabaab na majeshi ya serikali, maafisa wameeleza.

Mgogoro huo umejitokeza licha ya wito wa rais Sheikh Sharif Sheikh Ahmad kutaka kusitishwa mapigano katika kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhan.

Baadhi ya mapigano ya Jumamosi yalijikita zaidi katika barabara muhimu inayounganisha Mogadishu na mji wa Afgoye.

Afisa mmoja wa serikali alieleza kuwa wanamgambo 10 waliuawa. Waziri wa ulinzi wa Somalia, Yusuf Mohamed Siyad, siku ya Jumamosi alieleza kuwa idadi ya wanamgambo waliouawa ilikuwa haijajulikana.

"Waliondoka na kuacha wenzao wamekufa ingawa wengine waliwachukua. Pia waliwachukua wanamgambo wenzao waliojeruhiwa - kwasababu hiyo hatuna idadi yao kamili."

Barabara ya kuelekea Afgoye inatumika kusafirisha shehena kuelekea makambi ambako maelfu ya watu waliokimbia makazi yao wanaishi.

Uskochi yajitetea kumwachia al Megrahi


Serikali ya Uskochi imetetea uamuzi wake wa kumwachilia huru Abdelbaset Ali al-Megrahi, mtu aliyepatikana na hatia ya kulipua ndege ya Pan Am huko Lockerbie, huku ikikosolewa ndani na nje ya nchi.

Hatua hiyo inafuatia kauli kali kutoka kwa mkuu wa shirika la upelelezi la FBI, ambaye alisema kuachiliwa huru kwa Bw al-Megrahi iliwa ni kufanyia mzaha sheria.

Aliyewahi kuwa waziri kiongozi wa Uskochi, Jack McConnell alisema lilikuwa ni kosa kubwa la kiuamuzi.

Lakini waziri kiongozi wa sasa, Alex Salmond alisema kumwachilia huru Megrahi katika misingi ya huruma ulikuwa uamuzi sahihi.

Alisema Scotland ina uhusiano imara na wa kudumu na Marekani, "lakini haitarajiwi kila wakati tuwe tunakubaliana kwa kila jambo."

"Tunatambua kuwa kero. Tunatambua kutokubaliana. Lakini tunatakiwa kufanya kile kilicho sahihi kwa kuzingatia mfumo wetu wa sheria, hilo ndilo jambo tunalowajibika kulifanya," alisema.

Awali rais Barack Obama wa Marekani alisema hatua hiyo ilikuwa ni ''kosa'', na jamaa wa waathirika wa Marekani wamechukizwa na uamuzi huo.

Wengi wa watu 270 waliokufa katika ulipuaji wa ndege hiyo walikuwa ni Wamerekani.

Serikali ya Scotland imesema ilifanya mashauriano ya kina kabla ya Waziri wake wa Sheria, Kenny MacAskill kufanya uamuzi huo, kufuatia maombi ya Megrahi ya kuachiwa kwa sababu za kibinadamu au kuhamishiwa katika gereza la Libya.

Hata hivyo ushauri wa kidaktari ulikuwa unaonyesha kuwa Megrahi anategemewa kuwa amebakiza muda wa miezi mitatu tu kuishi.

Megrahi alipatikana na hatia ya mauaji ya kukusudia mwezi Januari mwaka 2001 katika kesi iliyoendeshwa chini ya sheria za Scotland nchini Uholanzi.

Moto mkubwa wateketeza Athens


Serikali ya Ugiriki imeelezea matumaini yake kwamba hatari ya moto ambao umekuwa ukiuzunguka mji mkuu wa Athens imeanza kupungua kutokana na kupwaya kwa nguvu za upepo.

Maelfu ya wakazi wa mji huo wameokolewa katika nyumba zao kufuatia moto wa msituni.

Karibu watu wote wa Aglos Stefanos, kilomita 23 kutoka kaskazini mashariki mwa Athens, walikimbia moto huo kwa magari au kwa miguu.

Moto umekuwa ukiteketeza eneo la kilomita 50 ukichochewa kwa upepo mkali usiotabirika.

Moto huo ambao ni mkubwa kuliko ule wa mwaka 2007 ulioua watu 70, unaelezewa kama ni angamizo kwa mazingira.

Juhudi za uzimaji moto zilisimamishwa wakati wa usiku giza lilipoanza kuingia siku ya Jumapili, huku moto huo ukiendelea kuwaka wakati wa usiku, ingawaje hakuna majeruhi walioripotiwa.

Mwelekeo wa upepo

Ingawa moto huo umeripotiwa kupungua katika maeneo ya mjini ulikuwa bado unaendelea kuteketeza zaidi maeneo ya misitu.

''Kubadilikabadilika kwa mwelekeo wa upepo kunatabiri moto huo'' msemaji wa kikosi cha zama moto Giannis Kapakis ameliambia shirika la habari la Reuters. ''Ni lazima wote tuwe watulivu katika kipindi cha usiku huu.''


Moto mkali Ugiriki
Hatari imeanza kupungua

Nyumba kadhaa zimeteketezwa na hali ya hatari imetangazwa katika eneo la mji wa Athens.

Waziri mkuu Costas Karamanlis amesema nchi inakumbana na ''mkasa mzito'' lakini akapongeza juhudi za waokozi kwa juhudi zao za kishujaa.

Italia, Ufaransa na Cyprus zimetuma ndege kusaidiana na vikosi vya zima moto vya Ugiriki.

Polisi wakiwa na vipaza sauti walizunguka katika eneo la Agios Stefanos mapema Jumapili kuwaasa wakazi kuelekea Athens mara moja.

''Tumekuwa tukiomba serikali tangu asubuhi kutuma vikosi'', amesema Panayiotis Bitakos makamu Meya wa eneo hilo. ''Muda umekwisha sasa, umekwisha sana.''




Takataka
Moto huo unaripotiwa kuwa umeanza siku ya Ijumaa katika eneo lililotengwa kutupa takataka la Grammatiko, karibu na mji mkongwe wa Marathon.

Unasambaa kwa kasi katika vilima nje ya mji wa Athens, ukiteketeza misitu.

Moto huo uliongezaka zaidi siku ya Jumamosi na kusambaa hadi Varnavas. Hadi siku ya Jumapili asubuhi nyumba zilikuwa zinaungua katika vitongoji vya Athens vya Drafi, Pikermi na Pallini.

Wakati wa usiku moto ulikumba kilele cha Pendeli, katika mwinuko, kitongoji cha kaskazini kinachoonyesha mandhari ya mji wa Athens, ukiteketeza majumba.

Sehemu kubwa ya mlima wa Pendeli iliteketezwa mwaka 2007, anasema Malcolm Brabant aliyeko Athens.

Miti iliyokuwa katika milima mitatu kati ya minne inayozunguka mjii mkuu Athens, ilishateketezwa katika matukio yaliyopita ya moto na mmomonyoko wa udongo katika misitu utakuwa ni wa kutisha, mwandishi wetu anaongeza.

Mkasa mzito

Mamia ya vikosi vya zima moto na wanajeshi vikisaidiwa kwa helikopta na ndege vimekuwa vikidondosha maji toka angani kuzima moto, lakini moto huo ulikuwa mkubwa kupindukia kuweza kudhibiti, mwandishi wetu anasema.

Gavana wa Athens Yiannis Sgouros ameiambia televisheni ya Ugiriki kuwa zaidi ya akari 30,000 za ardhi zimeteketezwa, katika kile anachokielezea kama ni ''maangamizi ya mazingira.''

Wakati wakazi wengi katika maeneo yaliyotishiwa na moto huo walifuata maelekezo ya kuhama, wengine walibaki wakijaribu kulinda nyumba zao.

Moto huo umesababisha moshi mzito katika anga la Athens.

Friday, August 21, 2009

Bingwa wa dunia wa mita 800 adhalilishwa


Bingwa wa dunia wa mbio za mita 800 Caster Semenya amedhalilishwa baada ya kutakiwa kufanyiwa uchunguzi juu ya jinsia yake, amesema mkuu wa idara ya michezo ya Afrika Kusini.
Leonard Chuene amesema bingwa huyo amechukuliwa kama vile ''mkoma''.

Mapema chama tawala nchini Afrika Kusini kiliwaasa wananchi kumuunga mkono na kumshangilia ''msichana wetu shujaa''.

Familia yake pia imesisitiza kuwa Caster Semenya ni mwanamke.
''Natambua kuwa ni mwanamke - nimemlea mwenyewe ,'' nyanya ya msichana huyo wa miaka 18 amesema.

Mama yake mzazi Dorcus Semenya ameliambia gazeti la Star kuwa, mashaka yaliyozuliwa juu ya jinsia ya mtoto wake yanatokana na ''wivu''.

''Iwapo utakwenda kijijini kwangu na kuuliza yeyote kati ya majirani zangu, watakueleza kuwa Mokgadi (caster Semenya) ni msichana,'' amesema.

''Wanajua kwasababu walinisaidia katika kumlea. Watu wanaweza kusema lolote wanalotaka lakini ukweli utabakia, kwamba mtoto wangu ni msichana. Sijali mambo kama hayo.''

Bwana Chuene, mkuu wa Idara ya Michezo Afrika Kusini amesema ataendelea kumtetea Semenya.

''Nitaendelea kufanya lolote lile, hata kama nitaondolewa Berlin, Ujerumani, lakini sitakubali kumwacha yule msichana adhalilishwe katika mtindo ambao amedhalilishwa, kwasababu hajafanya kosa lolote la jinai, '' amesema.

''Kosa lake lilikuwa ni kuwa amezaliwa jinsi alivyozaliwa.''

Katika taarifa ya chama tawala cha African National Congress (ANC) imeshutumu udadisi juu Semenya, aliyeshinda tuzo ya dhahabu katika mashindano dunia mjini Berlin hapo siku ya Jumatano, akiwaacha wapinzani wake wakichechemea.

''Maneno kama hayo yanaweza kuwawakilisha wanawake kama ni dhaifu,'' ANC imesema.

''Caster si mwanamichezo pekee wa kike mwenye umbo la kiume, na Shirikisho la Kimataifa la Wanamichezo lingetakiwa kulielewa hilo vyema zaidi,'' taarifa hiyo inasema.

Katika mahojiano na gazeti la Times la Afrika Kusini, nyanya wa bingwa huyo Maphuthi Sekgala mwenye umri wa miaka 80, amesema Semenya alikuwa akitaniwa alipokuwa mdogo kuwa ana muonekano wa kivulana.

Na pia alikuwa ni msichana pekee katika timu ya mpira wa miguu katika kijiji cha Fairlie, kilichopo katika jimbo la Limpopo kaskazini mwa Afrika Kusini.

''Iwapo utani huo ulikuwa ukimuumiza moyo, aliweka maumivu hayo moyoni na hakuonyesha hisia zake,'' amesema.

Tuesday, August 18, 2009

Shambulio kuelekea uchaguzi Afghanistan


Mshambuliaji wa mabomu ya kujitoa mhanga amelipua bomu na kuua watu saba katika msafara wa vikosi vya kijeshi vya nchi za magharibi, katika mjii mkuu wa Afghanstan.
Tukio la bomu hilo ambalo ni la pili katika muda wa siku tatu limekuja katika kipindi ambacho ulinzi umeimarishwa katika mji mkuu Kabul kwa ajili ya uchaguzi hapo siku ya Alhamis.

Kikosi kinachoongozwa na NATO kimesema taarifa zinaashiria kuwa baadhi ya wanajeshi wake ni miongoni mwa waliouawa na kujeruhiwa, wakati Umoja wa Mataifa umesema wafanyakazi wake wawili wameuawa.

Saa chache mapema, roketi ilirushwa kuelekea katika makazi ya rais mjini Kabul, lakini hakuna aliyeripotiwa kujeruhiwa.

Mashariki mwa nchi, wanajeshi wawili wa Marekani walikufa katika shambulio la bomu la barabarani, jeshi la Marekani limesema.

Na hapo siku ya Jumanne kusini mwa Afghanstan, katika jimbo la Uruzgan, wanajeshi wawili wa Afghanstan walikufa wakati mshambuliaji wa bomu la kujitoa mhanga mwenda kwa miguu alipojilipua katika kizuizi cha ukaguzi.

Rais Hamid Karzai anatarajiwa kuchaguliwa tena kama rais hapo siku ya Alhamis, ingawaje wawakilishi wanasema anakabiliwa na upinzani mkubwa kutoka kwa waziri wa zamani wa Mambo ya Nje Abdullah Abdullah. Wagombea kadhaa pia wanashiriki katika kinyang'anyiro hicho.

Hugh Sykes wa BBC mjini Kabul anasema matukio ya ulipuaji mabomu yanaelekea huenda yakawaogopesha watu kujitokeza kupiga kura.

Walioshuhudia wanasema shambulio hilo la Kabul lilitokea katika barabara yenye shughuli nyingi ya Jalalabad na kushambulia vikosi vya kijeshi vya kigeni karibu na soko lililojaa watu wengi, ambapo watoto waliikuwa ni miongoni mwa watu hamsini waliojeruhiwa.

Taliban wamedai kuhusika katika shambulio hilo.

Mwandishi mmoja aliyekuwako katika eneo la tukio aliwaona askari wa Uingereza waliokuwa wakifanya doria katika eneo hilo, wakikusanya kile kinachoonekana kuwa ni sehemu za miili ya binadamu kutoka katika paa la nyumba ya mtu mmoja muafghanistan.

''Niliona watu waliojeruhiwa na waliokufa wametapakaa kila mahali,'' muuza duka mmoja aitwaye Sawad ameliambia shirika la habari la Reuters.

Mlipuko huo ulisababisha moshi mzito angani, lakini haukuathiri sana mitaa yenye shughuli nyingi ya Kabul, anasema mwandishi wetu.

''Lilikuwa ni shambulio la kijitoa mhanga... Likilenga vikosi vya kijeshi vya kigeni,'' Mkuu wa police wa Kabul, Sayed Abdul Ghafar Sayedzada, aliliambia shirika la habari la AP.

Wafanyakazi wawili wa Umoja wa Mataifa wanaaminika kuuawa katika shambulio hilo.

''Nimestushwa na ninasikitika sana kutambua kuwa wawili kati ya wafanyakazi wangu ni miongoni mwa waliouawa katika shambulio la kujitoa mhanga la leo,'' mwakilishi maalum wa Umoja wa Mataifa Kai Eide alisema katika taarifa.

Vurugu hizi za karibuni zinakuja wakati uchunguzi wa BBC umeonyesha kuna ushahidi wa ukiukwaji wa kanuni za uchaguzi na ufisadi kuelekea siku ya uchaguzi wa rais.

Maelfu ya vitambuliho vya kupigia kura vimekuwa vikiuzwa na maelfu ya dola yamekuwa yakitolewa kama rushwa kununua kura.

Tume huru ya uchaguzi ya Afghanstan ambayo imekuwa ikisimamia mchakato wa uchaguzi imeshutumiwa kwa kushindwa kuzuia vitendo vitakavyoathiri uchaguzi.

Uchaguzi wa siku ya Alhamis utakuwa ni wa pili kumchagua rais tangu uvamizi ulioongozwa na Marekani mwaka 2001 ulioupindua utawala wa Taliban.

Marekani yazungumzia hatma ya Megrahi


Maseneta wa Marekani wanapinga kuachiliwa kwa mfungwa Abdelbaset Ali al-Megrahi aliyepatikana na hatia kushambulia kwa bomu ndege ya abiria huko Lockerbie katika anga ya Scotland.
Maseneta hao saba wamemhimiza waziri wa maswala ya sheria katika serikali ya Scotland kutomwachilia Bwana Megrahi ambaye ni raia wa Libya.

Megrahi, ndiye Mtu pekee aliyehukumiwa kwa shambulio hilo la ndege ya Pan Am 103, lililowaua watu 270 huko Lockerbie, mwaka 1988.

Maseneta hao, John Kerry na Edward Kennedy, Frank Lautenberg, Charles Schumer, Robert Menendez, Partick Leany na Kristen Gillibard wanadai kwamba kumuachilia huru Megrahi ni kinyume na jitihada za kupambana na ugaidi.

Waziri wa maswala ya kisheria wa Scotland Kenny MacAskill, anatarajiwa kuamua ikiwa Megrahi anayeugua saratani ataachiliwa au kurejeshwa nchini kwake Libya, chini ya mkataba wa ubadilishanaji wafungwa.

Mwaka uliopita, mawakili wa Megrahi waliwasilisha ombi la kuwachiliwa kwa dhamana katika mahakama ya rufa lakini ombi lake lilitupiliwa mbali.

Pendekezo la kumuachia Megrahi limepingwa vikali huko Marekani.

Kati ya abiria 270 waliokufa katika ndege hiyo ya Pan Am, 189 walikuwa raia wa Marekani.

Katika Barua waliomuandikia Bw. MacAskill, maseneta hao wa Marekani walimhimiza ahakikishe kwamba Megrahi anatimiza kifungo chake nchini Scotland.

Hillary Clinton, waziri wa mambo ya nchi za kigeni wa Marekani pia ameongeza uzito wake katika mvutano huu, akikariri kwamba Megrahi anastahili kumalizia kifungo chake Scotland.

Target Heart Rates


AHA Recommendation
Health professionals know the importance of proper pacing during exercise. To receive the benefits of physical activity, it's important not to tire too quickly. Pacing yourself is especially important if you've been inactive.

Target heart rates let you measure your initial fitness level and monitor your progress in a fitness program. This approach requires measuring your pulse periodically as you exercise and staying within 50 to 85 percent of your maximum heart rate. This range is called your target heart rate.

What is an alternative to target heart rates?

Some people can't measure their pulse or don't want to take their pulse when exercising. If this is true for you, try using a "conversational pace" to monitor your efforts during moderate activities like walking. If you can talk and walk at the same time, you aren't working too hard. If you can sing and maintain your level of effort, you're probably not working hard enough. If you get out of breath quickly, you're probably working too hard — especially if you have to stop and catch your breath.

When should I use the target heart rate?

If you participate in more-vigorous activities like brisk walking and jogging, the "conversational pace" approach may not work. Then try using the target heart rate. It works for many people, and it's a good way for health professionals to monitor your progress.

The table below shows estimated target heart rates for different ages. Look for the age category closest to yours, then read across to find your target heart rate.

Age Target HR Zone
50–85 % Average Maximum
Heart Rate
100 %
20 years 100–170 beats per minute 200 beats per minute
25 years 98–166 beats per minute 195 beats per minute
30 years 95–162 beats per minute 190 beats per minute
35 years 93–157 beats per minute 185 beats per minute
40 years 90–153 beats per minute 180 beats per minute
45 years 88–149 beats per minute 175 beats per minute
50 years 85–145 beats per minute 170 beats per minute
55 years 83–140 beats per minute 165 beats per minute
60 years 80–136 beats per minute 160 beats per minute
65 years 78–132 beats per minute 155 beats per minute
70 years 75–128 beats per minute 150 beats per minute

Your maximum heart rate is about 220 minus your age. The figures above are averages, so use them as general guidelines.

Note: A few high blood pressure medications lower the maximum heart rate and thus the target zone rate. If you're taking such medicine, call your physician to find out if you need to use a lower target heart rate.

How should I pace myself?

When starting an exercise program, aim at the lowest part of your target zone (50 percent) during the first few weeks. Gradually build up to the higher part of your target zone (75 percent). After six months or more of regular exercise, you may be able to exercise comfortably at up to 85 percent of your maximum heart rate. However, you don't have to exercise that hard to stay in shape.

Homa ya nguruwe yaenea Kenya


Taarifa kutoka Kenya na Jamhuri ya kidemocrasia ya Congo zinathibitisha kuwepo na kuenea kwa homa ya nguruwe katika nchi hizo mbili .
Taarifa hizi zimethibishwa na mawaziri wa afya wa nchi hizo Bi Beth Mugo na Bw. Augustin Mopipi. Nchini Kenya, Bi Mugo aliiambia BBC kwamba wizara yake imethibitisha kwamba maambukizi ya homa ya H1N1 yamekuwa yakitokea katika maeneo mbali mbali. Kufikia sasa watu wapatao 71 wamethibitishwa kuugua homa hiyo.

Kati ya hao, amesema watu 40 wameambukizwa homa hiyo katika mji mkuu wa Kenya Nairobi na watu wengine 10 huko Keiyo magharibi mwa nchi hiyo, ambako watu 300 wanaendelea kuchunguzwa baada ya kupatikana na dalili za homa hiyo.

Kati ya maeneo mengine yalioathrika nipamoja na mji wa Kisumu ambako watu 18 wameambukizwa, mjini Garissa watu wawili na Mjini Nyeri mtu moja.

Licha ya maambukizi hayo, waziri Mugo amewashauri wakenya wasiwe na hofu, huku akisisitiza kwamba Homa hiyo inadhibitiwa na haina makali kama ilivyo hofiwa hapo awali.

Wanaoambukizwa hata hivyo wamelalamika kwamba hawapati dawa.

DR Congo

Huko Congo serikali pia imethibitisha kwamba mtu moja ameambukizwa homa hiyo kusini mashariki mwa nchi hiyo.

Hii ni mara ya kwanza homa hiyo kuthibitishwa nchini humo kwani ripoti za hapo awali zilizodai kuwepo homa hiyo zilikanushwa baadaye.

Bwana Mopipi akizungumza na BBC, alithibitisha kwamba mtu anayeugua ni mchimba madini kutoka mji wa Lumbubashi, katika jimbo la Katanga, aliyekuwa amesafiri Afrika Kusini.

Mchimba madini huyo waziri alisema ametengwa pamoja na wote waliosafiri naye licha ya kwamba hawajaonesha dalili zozote za kuugua homa hiyo.

Bwana Mopipi amesema kwamba, serikali ya Jamhuri ya kidemocrasia ya Congo ilikuwa tayari kupambana na homa hiyo na imeweka hifadhi ya madawa ya kutosha.